Na.Frank
Mvungi-Maelezo
Serikali kununua meli
mpya ili kuongeza tija katika utoaji wa
huduma za usafirishaji ndani ya Ziwa Victoria.
Akizungumza wakati wa
kipindi cha Tunatekeleza kinachorushwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC)
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi ) Dkt.
Leonard Chamuriho alisema kuwa ujenzi wa meli hiyo ni utekelezaji wa ahadi ya
Serikali kwa wakazi wa Kanda ya Ziwa.
“Bajeti yetu ni
takribani trilioni 2.5 hivyo, inatuwezesha kutekeleza mikakati yetu ya kuhakikisha
kuwa sekta ya uchukuzi inachochea ujenzi wa uchumi wa Viwanda nchini”Alisisitiza
Dkt. Chamuriho.
Akizungumzia mikakati
yakuendeleza sekta hiyo Dkt. Chamuriho alisema kuwa Bajeti waliyotengewa
inawawezesha kuanza ujenzi wa reli kwa viwango vya Kimataifa (Standard gauge) ambayo
itajengwa kwa awamu tano ambapo awamu ya
kwanza itahusisha eneo la Dar es salaam na Morogoro.
Pia alifafanua kuwa ,upanuzi
wa bandari ya Dar es salaam, Mtwara na Mwanza utachochea ukuaji wa uchumi hasa
katika eneo la Bandari ya Mtwara
itochochea ukuaji wa Sekta ya gesi na Viwanda.
“Jambo Jingine ni
kukarabati meli zote katika ziwa Victoria na Tanganyika ili kusaidia kuboresha
usafirishaji wa abiria na mizigo katika maeneo mbalimbali” alisisitiza Dkt.
Chamuriho.
Aidha Dkt.Chamuriho
alibainisha kuwa Serikali imepanga kujenga Bandari ya Bagamoyo kwa kuwatumia
wawekezaji ili kuchochea ukuaji wa uchumi wa Viwanda katika eneo la Bagamoyo na
maeneo mengine kwa kuwa itatumika kusafirisha bidhaa zinazozalishwa na
malighafi kutoka nje ya nchi kwa ajili ya viwanda.
Katika hatua hiyo Dkt
Chamuriho alisema kuwa Mikakati mingine iliyopo ni kuimarisha shirika la ndege
Tanzania (ATCL) kwa kufunga mfumo madhubuti wa kielektroniki utakaosaidia
kuondoa tatizo la upotevu wa mapato hali itakayochangia kukuza shirika hilo kwa
manufaa ya Taifa.
Sekta ya uchukuzi ni
mhimili wa ujenzi wa Uchumi wa Viwanda hapa nchini kwa kuwaungainisha
wazalishaji wa bidhaa, malighafi na wananchi katika maeneo mbalimbali ndani na
nje ya nchi.
No comments:
Post a Comment