Habari za Punde

Tanesco yawatoa hofu wateja wake, wasema Gridi ya Taifa ipo salama


Kaimu Meneja Mwandamizi udhibiti mifumo ya umeme TANESCO makao makuu, Mhandisi Abubakar Issa,(katikati), akionyesha kifaa kilicholipika (female connector), cha umeme wa 132kv kutoka Ubungo kwenda Chalinze. Kulia ni KaimunMeneja Uhusiano, Bi. Leila Muhaji na kushoto ni mwangalkizi mkuu wa kituo cha kupoza umeme cha Ubungo jijini Dar es Salaam, Bw,Deodatus Ngwanda


NA K-VIS BLOG/Khalfan Said

SHIRIKA la Umeme Tanzania, (TANESCO), limeeleza chanzo cha kukatika umeme leo Januari 25, 2017), ni kulipuka kwa kikata umeme,(Circuit breaker), baada ya kifaa kijulikanacho kama female connector ya umeme wa 132kv kutoka kituo cha kupoza umeme cha Ubungo jijini Dar es Salaam kwenda Chalinze mkoani Pwani kupata hitilafu.

"Napenda kuwahakikishia wateja wetu kuwa gridi ya taifa iko salama, hakuna tatizo lolote isipokuwa ilizima baada ya kikata umeme hicho kulipuka, lakini sasa mambo yamewekwa sawa na umeme unazidi kurejea katika hali yake ya kawaida kote nchini" alisema Mhandisi Issa, wakati waandishi wa habari walipopelekwa kujionea wenyewe hitilafu hiyo majira ya mchana leo. 



Hata hivyo alisema kifaa kilichoharibika kinasafirishwa kutoka mkoani Tanga, na mara kitakapowasili kitafungwa mahala kilipoharibika kile cha awali.
 Hii ndiyo kikata umeme (Circuit breaker) iliyolipuka
 Female Connector inayotoa umeme hapo ubunge kupeleka Chalinze mkoani Pwani ambayo ililipuka
 Female connector (juu katikati) iliyolipuka
 Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO makao makuu, Bi Leila Muhaji, akiwa na baadhi ya waandshi wa habari waliotembelea eneo hilo leo mchana Januari 25, 2017




No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.