Na Woinde Shizza,Arusha
Wakuu wa Mashirika ya Umeme kutoka katika Nchi kumi za Afrika zinazozalisha
Umeme(Eastern Africa Power pool(EAPP)
zimekutana jijini Arusha kwa malengo ya kujadili mfumo wa usafirishaji wa umeme ikiwa ni pamoja na namna ya wananchi wao watakavyoweza pata nishati ya umeme kwa uraisi tofauti
na sasa.
Hayo yalisemwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini
Dkt.Juliana Palangyo alipokuwa akizungumza katika ufunguzi wa mkutano huo wa Wakuu wa Mashirika ya Umeme katika Nchi hizo za Eastern Africa Power Pool (EAPP) mapema leo.
Dkt.Palangyo alisema kuwa lengo halisi ni kuweza kujadili mambo mbalimbali yahusuyo na nishati ya umeme kwa watumiaji wake kwani kuna
uwezekano mkubwa wa nchi zote zilizo kwenye umoja huo.
Alisema kwa sasa yapo baadhi ya makampuni ambayo yalikuwa yanauza
umeme kwa gharama kubwa hasa kwa wananchi ambao hawajapata huduma hiyo ya umeme lakini kupitia umoja huo wataweza kupata nishati hiyo kwa gharama
nafuu.
"Hizi nchi za eastern tumekutana hapa ili tujadili namna ambayvo tunayvoweza kutafuta namna ya kuzalisha umeme kwa bei nafuu na kisha nchi hiyo itaweza kuuza umeme kwa bei ndogo"aliongeza Dkt.Palangyo.
Hata hivyo kwa upande Kaimu Meneja Uhusiano wa Shirika la Tanesco Bi.leila Muhaji alisema kuwa katika mkutano huo pia watajadili namna ambavyo Tanzania itajenga njia ya usafirishaji wa umeme wa njia ya maji ambayo itatoka nchi ya Tanzania kwendas Kenya,Zambia,pamoja na nchi
nyingine
Muhaji alisema kuwa Tanzania itanufaika na ujenzi wa njia hizo hivyo
jamii itanufaika kwa kiwango kikubwa sana kama ilivyo kwenye nchi ambazo zimeendelea duniani.
"Hata hivyo mara baada ya huu mkutano wa wakuu wa nchi zinazolisha umeme tunatarajia pia kuwepo na wadau wengine ambao ni mawaziri kutoka nchi zote ambao nao sasa wataweza kuweka mambo sawa ili huduma hii iweze kumfikia mlengwa"aliongeza Muhaji
Alimalizia kwa
kutaja nchi ambazo zina unda umoja huo kuwa ni Tanzania
,Kenya,Uganda ,Rwanda ,Burundi ,Sudan , Congo, Ethiopia ,Djbout,
Libya pamoja na Egypt.
No comments:
Post a Comment