Habari za Punde

Mvua kubwa za masika Pemba zasababisha maporomoko ya ardhi na madaraja kukatika

 MITI mbali mbali ikiwa imeanguka katika moja ya sehemu ya Barabara ya Chake-Mkoani, kufuatia mvua kubwa iliyonyesha Kisiwani Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 MAGUNIA 518 ya Karafuu Kavu zikiwa hazikuharibika katika ghala la kuhifadhia karafuu la Shirika la ZSTC Mkoani, baada ya ghala hilo kuanguka sehemu ya Ukuta na gunia tisa kufukiwa na dongo zikiwa na karafuu kavu.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 SEHEMU ya Ghala la Kuhifadhia karafuu la ZSTC Mkoani, likiwa limebomoka baada ya kuangukiwa na mti uliokuwa katika mlima na kupelekea Gunia Tisa za Karafuu Kavu zenye thamani ya Zaidi ya Milioni 5 kufukiwa na dongo kutokana na mvua kubwa iliyonyesha Kisiwani Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 WATOTO wadogo wakisafisha kwa kutoa dongo nje katika Msikiti wa Mbuyuni Wilaya ya Mkoani, baada ya sehemu kubwa ya msiki huo kuangukiwa na Udongo ulioporomoka na kuharibu Msikiti, kama unavyoonekana katika Picha.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 WATOTO wadogo wakisafisha kwa kutoa dongo nje katika Msikiti wa Mbuyuni Wilaya ya Mkoani, baada ya sehemu kubwa ya msiki huo kuangukiwa na Udogo ulioporomoka na kuharibu Msikiti, kama unavyoonekana katika Picha.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 WANANCHI wa Mbuyuni Wilaya ya Mkoani, wakitoa msaada kwa kuondosha Udongo, ili kutoa Vitu vilivyofukiwa na Fusi baada ya Nyumba ya Fadhil Amour Mohamed kuangukiwa na Udongo na kutokupata hata kitu Kimoja.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 MOJA ya nyumba wanazoishi wananchi katika shehia ya Mbuyuni Wilaya ya Mkoani, ikiwa imeelemewa na Udongo uliokatika katika mlima, uliopelekea nyumba hiyo kuvunjika sehemu ya Ukuta huo, kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha Kisiwani Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 KIJIKO cha Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Pemba, kikiondosha dongo lililoporomoka katika milima na kuingia barabarani, kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha Kisiwani Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 ZAIDI ya Mita 150 katika barabara ya Mgagadu Kiwani eneo la Darajani, likiwa limeharibiwa Vibaya na Mvua zinazoendelea Kunyesha Kisiwani Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 VIONGOZI mbali mbali wa Serikali wakiongoza na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Mhe:Mwanajuma Majid Abdalla, wakikagua sehemu ya barabara ya Mgagadu Kiwani Ilivyoharibika kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha Kisiwani Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, 
 MATUMAINI ya wananchi kupata kilimo chao cha mpunga walichokilima kwa muda mrefu yameanza kupotea, kufuatia mashamba ya kilimo hicho kujaa maji mengi kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha Kisiwani Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 MIONGONI mwa Nymba 58 za wananchi wa shehia ya Mwambe Wilaya ya Mkoani, zilizoharibiwa na mvua zinazoendelea kunyesha kisiwani Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 MVUA zinazoendelea kunyesha Kisiwani Pemba, zimeanza kuleta madhara kwa wananchi wanaoishi, Pichani baadhi ya vitu vya mmoja wa wananchi wa Shehia ya Wambaa vikiwa nje baada ya nyumba yake kujaa maji.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA

 VIONGOZI mbali mbali wa Serikali wakiongoza na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Mhe;Mwanajuma Majid Abdalla, akiwangalia daraja la Pujini lililowatenganisha wananchi wa Pujini na Chake Chake baada ya sehemu ya barabara hiyo kukatika, kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha Kisiwani Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 WANANCHI wa Kipapo Mgelema wako hatarini kukosa barabara ya kupita baada ya mvua kubwa iliyonyesha Kisiwani Pemba, kuharibu barabara yao.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

1 comment:

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.