STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 26.04.2017
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri
Jeshi Mkuu Dk. John Pombe Mgafuli amewahakikishia wananchi wa Tanzania kuwa
yeye na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed
Shein wataendelea kuulinda Muungano kwa nguvu zao zote.
Rais Magufuli aliyasema
hayo leo huko katika uwanja wa Jamhuri, Dodoma katika sherehe za kuadhimisha
miaka 53 ya Mungano wa Tanganiyika na Zanzibar, sherehe zilizohudhuriwa na
maelfu ya wananchi pamoja na viongozi mbali mbali wa Serikali na vyama vya
siasa akiwemo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali
Mohamed Shein.
Katika hotuba yake Rais
Magufuli alitoa pongezi kwa Watanzania wote kwa kutimiza miaka 53 ya Muungano wa
Tanganyika na Zanzibar na kusisitiza kuwa leo ni siku ya kihistoria na ni
‘Birthday’ ya Tanzania nzima.
Alisema kuwa siku kama
ya leo miaka 53 iliyopita waasisi wa Taifa hili Marehemu Mwalimu Julius
Kambarage Nyerere na Hayari Mzee Abeid Amani Karume walifanya kitendo hicho cha
kihistoria ambacho kimeweza kuendelezwa na viongozi wote waliofuatia katika
uongozi wao nchi hii na kusema kuwa kwa upande wao na wao watahakikisha
Muungano unadumu.
Alieleza kuwa kabla ya
ukoloni mashirikiano makubwa yalikuwepo baina ya watu wa Zanzibar na Tanganyika
sambamba na mashirikiano na uhusiano mwema wa vyama vya siasa vilivyopigania
ukombozi ambavyo ni TANU na ASP na baada ya uhuru haikuwa vigumu kuunganisha
nchi mbili hizo.
Aliongeza kuwa katika
miaka 53 ya Muungano mafanikio makubwa yamepatikana ya kiuchumi, kisiasa na
kijamii sambamba na kuendeleza amani, uhuru na umoja hali ambayo imepelekea
kulindwa vyema kwa mipaka ya Tanzania.
Alisema kuwa Serikali
zote mbili ya Jamhur ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar zimefanya juhudi kubwa kukuza uchumi na kuimarisha maendeleo pamoja na
kukuza demokrasia na kueleza kuwa Tanzania ya leo ni tofauti na ile ya mwaka
1964.
Rais Magufuli alieleza
kuwa kutokana na mafanikio hayo, Tanzania imeweza kushiriki katika ukombozi wa
nchi mbali mbali ndani ya Bara la Afrika na nje ya Bara la Afrika na kuongeza
kuwa zipo nchi nyingi zinazojaribu kuungana lakini zimeshindwa.
“Kuulinda Muungano si
jambo rahisi kwani hata ndoa zetu kuzilinda ni tabu kubwa… na atakaejaribu
kuuvunja Muungano huu atavunjwa yeye”,alisema Rais Magufuli.
Aidha, aliwataka
Watanzania kufikiria walipotoka, walipo na wanapoelekea na kuleza kuwa katika
kizazi kilipo hivi sasa wengi wao wamezaliwa baada ya Muungano huo hivyo ni
vyema ukaendezwa, ukatunzwa na kulindwa kwa nguvu zote.
Sambamba na hayo,
alisema kuwa licha ya kuwepo mafanikio bado kuna baadhi ya changamoto ndani ya
Muungano huo ambapo kwa kupitia Kamati maalum iliyoundwa kwa alengo la kutatua
changamoto hizo chini ya Mweneykiti wake Makamo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Samia Suluhu Hassan zinafanyiwa kazi.
Katika sherehe hizo mapema
Amiri Jeshi Mkuu alikagua Gwaride na baadae lilipita mblele yake pole pole na kwa
mwendo wa haraka na kusonga mbele hatua 15 kwa ajili ya kutoa salamu ya Utii
kwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu.
Kikundi cha Makomandoo
kilionyesha ukomandoo wao na kuonesha jinsi walivyokomaa kijeshi na kikamandoo
na kutoa budurani kwa viongozi na wananchi jinsi ya kujilinda katika mapambano
sambamba najinsi ya kupambana na adui kwa kutumia miili yao.
Onesho la Mbwa na Farasi
nalo lilitia fora pamoja na Halaiki ya vijana wa Skuli za Sekondari mjini
Dodoma na kufuatiwa na vikundi maalum vya ngoma za asili nazo zilitumbuiza,
Kwaya ya Makongoro kutoka Mwanza na Bendi ya Muziki wa Kizazi Kipya kutoka
Yamoto Bend nacho kilitumbuiza uwanjani hapo.
Ndege za kivita
zilionesha umahiri wake mbele ya Amiri Jeshi Mkuu na kuwa ndio kitendo cha
mwisho kilichofunga sherehe hizo zilizofana kwa kiasi kikubwa huku umma wa
wananchi wakishangiria kwa nderemo na vigeregere.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment