NA HAJI NASSOR, PEMBA
MAMLAKA ya Usimamizi wa Bima Tanzania
‘TIRA’ imesema sasa imefika mwisho wa mawakala na makampuniza na uuzaji wa bima
za vyombo vya moto zisizotambulika ‘feck’, bada ya Mamlaka hiyo, kuwa na njia
za kielektroniki za uhakikiwa bima hizo.
Mmlaka
hiyo imesema, kwa muda mrefu wamiliki wa vyombo vya moto, wamekuwa wakiuziwa
bima zisizostahiki bila ya wao kujua, ingawa kwa sasa kwa wauzaji hao, mwisho
wao umefika.
Akizungumza
kwenye mafunzo ya siku moja, yaliowahusishwa askari wa kikosi cha usalama barabarani na kufanyika skuli ya
sekondari Madungu Chakechake, Mkurugenzi wa Masoko na utafiti wa Mamlaka hiyo
Adelaida Muganyizi alisema sasa bima zote zitahakikiwa kwa njia ya kielektroniki.
Mkurugenzi
huyo alieleza kuwa, kwa vile kisheria kila kampuni au wakala wa kuuza bima
anatakiwa awe amesjaliwa na Mamlaka ya usimamizi wa bima Tanzania ‘TIRA’
itakuwa ni rahisi kuwashika wale mawakala wanaofanyakazi zao kimagumashi.
Alieleza
kuwa, kupitia mfumo wa kisasa wa kuandika neno stika ikifuatiwa na namba ya
bima na kuituma kwenda namba 15200, kwa milikiwa gari au chombo cha moto
atagundua uhalali wa wakala huyo.
“TIRA
baada ya kukaa na wataalamu sasa imekuja na mfumo wa kidigitaji kwa anaenunua
bima kabla ya kulipa, atafuata maelekezo hayo na kutuma kwenye namba husika, na
hapo sasa atagundua kuwa muuza bima huyo anatambuliwa na ‘TIRA’ au ni wa
mitaani”,alieleza.
Kwa
upande wake Menaja wa ‘TEHAMA’ wa Mamlaka hiyo Aron Malaki alisema, kazi iliopo
mbele yao kwa sasa, ni kutoa elimu kwa wamiliki wa vyombo vya moto na wananchi
wengine, juu ya kufuata mfumo huo wa kisasa.
“Faida
yake hasa kwa abiria, iwapo gari haina bila halali ni vigumu unapopata ajali au
kukugongwa kupata fidia kutokana na mauimivu ulioyapata kwa vile uhalali wa
bima haupo”,alifafanua.
Mapema
baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wa siku moja, wameiomba ‘TIRA’ kuhakikisha
elimu hiyo wanaisambaaza kwa jamii nzima, ili kuhakikisha inawafikia.
Hata
hivyo walisema kwa sasa wataondokana na ile njia ya zamani ya kukagua bima kwa
kuangalia rangi na tarehe iliokatwa au kumalizika, na sasa kwa kutumia mfumo wa
kisasa watafanyakazi wa uweledi.
No comments:
Post a Comment