Habari za Punde

Balozi Seif Amjulia Hali Mwakilishi wa Jimbo la Uzini Zanzibar Mhe Raza Nyumbani Kwake Kibweni Zanzibar.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kulia akimfariji Mwakilishi wa Jimbo la Uzini Mh. Mohamed Raza Hassanali hapo Hotelini Kwake Golden Tulip Kibweni nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.Mh. Raza anaendelea na mapumziko mafupi baada ya kufanyiwa matibabu Nchini India hivi karibuni.Aliyepo nyuma yao ni Mdogo wake Mh. Mohamed Raza ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Kimbesamaki Mh. Ibrahim Raza.
Mwakilishi wa Jimbo la Uzini Zanzibar Mhe. Mohamed Raza kati kati akieleza namna alivyopata huduma za Afya wakati akiwa Hospitalini Nchini India. Wa kwanza kulia ni Balozi Seif na kulia ya Mheshimiwa Raza ni Daktari Azan anayefuatilia afya yake katika kipindi hichi cha mapumziko.

Dr. Azan akimueleza Balozi Seif baadhi ya njia anazopaswa Mtu kuzichukuwa  katika kujilinda dhidi ya maradhi ya Kisukari makubwa zaidi ni kufuata miko ya vyakula na kufanya mazoezi kila siku.
Dr. Azan akimueleza Balozi Seif baadhi ya njia anazopaswa Mtu kuzichukuwa  katika kujilinda dhidi ya maradhi ya Kisukari makubwa zaidi ni kufuata miko ya vyakula na kufanya mazoezi kila siku.(Picha na – OMPR – ZNZ.)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.