Mbarouk Songoro, Bingwa Mtetezi wa Mbio za Baiskeli akiwa akielekea Kojani kuungana na Team Rafiki iliyopiga kambi Kisiwa cha Kojani kwa madhumuni ya kutafuta vipaji vya waogeleaji.
Ali Othman Ali, Pemba
Maandalizi ya Tamasha la kimichezo
kisiwani Pemba linalojulikana kama Pemba weekend Bonanza yanazidi kufana ambapo
timu ya Rafiki network inaendelea kusaka vipaji
vya washiriki katika michezo mbali mbali.
Tarehe 23 Julai 2017 Timu ya Rafiki network iliwasili katika kisiwa cha
Kojani kwa ajili ya kusajili vijana wenye uwezo wakushiriki mashindano ya kuogelea.
Jumla ya waogeleaji tisa kutoka kisiwa
cha kojani wamethibitisha kushiriki katika
mashindano hayo ambayo yamepangwa kufanyika katika fukwe za vumawimbi siku ya
tarehe 30 Julai 2017.
Akizungumza na washiriki hao mara baada
ya kuwasili katika kisiwa cha kojani Mratibu wa Matukio na Matamasha wa Kampuni
ya Rafiki Network Nd. Salim Jabu Dawa
amesema ingekua si busara kufanya
mashindano ya kuogelea kisiwani Pemba bila kushirikisha waogeleaji kutoka kisiwa
cha Kojani.
“Tumeamua kuja hapa kojani kusaka vipaji
vya waogeleaji kwani ingekua sibusara kufanya mashindano haya bila kuishirikisha waogeleaji kutoka kisiwa cha kojani” amesema Mratibu
wa Matukio na Matamasha wa Kampuni ya
Rafiki Network Nd. Salim Jabu Dawa.
Tamasha hilo la Kimichezo linatarajiwa
kuzinduliwa rasmi siku ya Ijumaa tarehe 28 Julai 2017 kwa mchezo wa Ng’ombe
utakaofanyika chwale mbapo siku ya Jumamosi ya tarehe 29 Julai resi za baiskeli
hatua ya mchujo zitafanyika zikijumuisha washiriki 67 na siku ya Jumapili Julai
Tamasha litafikia kilele kwa kushuhudia resi za baiskeli mzunguko wa pili
utakao wakutanisha washiriki 30.
Siku hiyo ya kilele cha tamasha jumla ya
waogeleaji 70 wataonesha umahiri wao kabla ya Mchuano mkali wa Ngalawa ambapo jumla ya Ngalawa 23 kutoka maeneo
mbali mbali kisiwani Pemba zitachuana.
No comments:
Post a Comment