Katibu Mkuu Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante
Ole Gabriel (kushot) akimsikiliza
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka (kulia) alipofanya ziara ya kutembelea Mkoa huo.Picha
na Zawadi Msalla-WHUSM.
Na
Zawadi Msalla-WHUSM
Mkuu
wa Mkoa wa Njombe Mhe. Christopher Ole Sendeka amewataka watendaji wa Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa
na Michezo kuwa mstari wa mbele katika kutoa elimu kwa umma ya kuwa na utamaduni wa kutumia muda
kimkakati ili kufanya kazi kwa bidii na kufikia
malengo.
Ayasema
hayo wakati wa mkutano na watendajin hao walipomtembelea ofisini kwake wakati wa ziara
ya kutembelea mikoa ya kusini mwa Tanzania kwa lengo la kutembelea maeneo
mbalimbali yanayojihusisha uhifadhi wa utamaduni usioshikika kama vile mila na
desturi za Watanzania.
“Utamaduni
wa kutumia muda kimkakati ni muhimu kwa Taifa na mtu binafsi kwa kuwa inasaidia
katika kuweka motisha ya kufanya kazi kwa bidii na hivyo kufikia lengo
lililokusudiwa” alisema Mhe. Ole Sendeka.
Aidha
aliongeza kwa kueleza kuwa falsafa ya mabadiliko ya utamaduni chanya ya
ufanyaji kazi ilianza tangu awamu ya kwanza ya uongozi wa Mwl. Nyerere
iliyokwenda kwa jina la Uhuru na Kazi na baadaye ikifuatiwa na kazi ni kipimo
cha Utu ambapo katika utawala wa awamu hii ya tano inaongozwa na hapa kazi tu
lengo ikiwa ni kufanya kazi kwa ajili ya kukuza uchumi wetu.
Mhe.
Ole Sendeka anaeleza kuwa dhumuni za falsafa hizo ni kuhakikisha kuwa kila mtu
anatimiza wajibu wake wa kutumia muda kimkakati kwa kufanya kazi ili kujenga Taifa
bora lenye maendeleo.
“Endapo
elimu ya kutosha ya utamaduni wa kufanya kazi itatolewa ni imani kuwa azma ya
Mhe. Rais ya kuwatoa watanzania katika uchumi ulio nyuma na tegemezi kwa kuwapeleka
katika uchumi wa kisasa wa taifa linalojitegemea itawezekana” alisema Mhe. Ole
Sendeka.
Kwa
upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof.
Elisante Ole Gabriel aliahidi kufanyia
kazi mawazo hayo kwa kuhakikisha jamii inapata elimu ya kutosha namna ya kuwa
na utamaduni wa kutumia muda kimakakati kwa kufanya kazi kwa bidii ili kufikia
malengo yaliyokusudiwa.
Pia alieleza kwamba ni kweli usiopingika ili Taifa liweze kufikia uchumi wa viwanda ni budi kwa
wananchi wake kujengea utamaduni wa kufanya kazi kwa bidi ikiwemo kutumia muda
kimkakati.
No comments:
Post a Comment