Habari za Punde

Zijuwe Timu 12 Zitakazoshiriki Ligi No 1 na 16 Ligi No 2 Zanzibar.

Na: Abubakar Khatib Kisandu, Zanzibar.
Msimu mpya wa mwaka 2017-2018 kutakuwa na ligi one na ligi two ambapo ligi one ndio ya juu kabisa yani Primier ligi na ligi two itakuwa daraja jipya kwa Zanzibar.

Ligi hizo zote zitatoa wawakilishi wa Zanzibar katika Mashindano ya Kimataifa, ambapo Ligi one itatoa muwakilishi wa Kombe la Klabu Bingwa Barani Afrika wakati ligi two itatoa muwakilishi wa Kombe la Shirikisho Barani humo.

Timu hizo 12 zilizofanikiwa kucheza ligi kuu (Ligi 1) msimu mpya wa mwaka 2017-2018 ni JKU, Jang’ombe Boys, Zimamoto, Taifa ya Jang’ombe, Polisi, KMKM kwa upande wa Unguja na Pemba ni Jamhuri, Kizimbani, Mwenge, Okapi, Chipukizi na New Stars.

Kwa upande wa timu 16 zitakazocheza ligi 2 msimu mpya wa mwaka 2017-2018 kati ya hizo 8 za Unguja na 8 za Pemba ambapo za Unguja ni Mafunzo, KVZ, Black Sailors, Chuoni, Kilimani City, Kipanga, Miembeni City na Charawe wakati za Pemba ni Dogomoro, Wawi Star, Shaba, Young Islander, FSC, Hardrock, Chuo Basra na Opek.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.