Habari za Punde

Rais Dk Shein azungumza na ujumbe wa bodi ya wakurugenzi shirika la nyumba, uongozi wa wizara ya ujenzi, mawasiliano na usafirishaji

  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akionesha Ramani ya Ujenzi wa Mji wa kisasa utakaojengwa  sambamba na ufukiaji wa Bahari ya  Eneo la pwani ya Gulioni  katika kikao cha siku moja kilichojumuisha  Uongozi wa Wizara ya Ujenzi,Mawasiliano na Usafirishaji pamoja na Wajumbe  wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Nyumba na Uongozi wa Shirika la Nyumba  katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo,[Picha na Ikulu.] 01 /08/2017.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akionesha Ramani ya Ujenzi wa Mji wa kisasa utakaojengwa  sambamba na ufukiaji wa Bahari ya  Eneo la pwani ya Gulioni  katika kikao cha siku moja kilichojumuisha  Uongozi wa Wizara ya Ujenzi,Mawasiliano na Usafirishaji pamoja na Wajumbe  wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Nyumba na Uongozi wa Shirika la Nyumba  katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo,[Picha na Ikulu.] 01 /08/2017.
 Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Nyumba wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) wakati alipofanya kikao cha siku moja pamoja na Uongozi wa Wizara ya Ujenzi,Mawasiliano na Usafirishaji katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo,[Picha na Ikulu.] 01 /08/2017.


 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) alipokuwa akizungumza na  Uongozi wa Wizara ya Ujenzi,Mawasiliano na Usafirishaji pamoja na Wajumbe  wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Nyumba na Uongozi wa Shirika la Nyumba  katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo,[Picha na Ikulu.] 01 /08/2017.


STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
  Zanzibar                                                                 01.08.2017
---
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, amesema kuwa kuwepo kwa mabadiliko makubwa ya kimaendeleo baada ya kuundwa kwa Mamlaka ya Viwanja vya ndege vya Zanzibar kumeweza kuongeza mapato na kuahidi kuimarika zaidi hali hiyo ndani ya kipindi chake cha uongozi.

Dk. Shein aliyasema hayo leo, alipokutana na uongozi wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji, Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege pamoja na Uongozi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege katika vikao vinavyoendelea Ikulu mjini Zanzibar.

Dk. Shein alitumia fursa hiyo kuipongeza Mamlaka hiyo kwa kufanya mabadiliko makubwa katika viwanja vya ndege vya Zanzibar hatua ambayo imeweza kusaidia kwa kiasi kikubwa ongezeko la mapato katika viwanja hivyo.

Katika maelezo yake Dk. Shein alisema kuwa licha ya baadhi ya changamoto zilizopo lakini Mamlaka imeweza kupata mafanikio makubwa na hivi leo viwanja vya ndege Unguja na Pemba viweza kuimarika na kuleta tija kwa kuongeza mapato.

Akizungumza suala zima la fidia kwa wananchi waliojenga pembezoni mwa uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar Dk. Shein alisema kuwa ni vyema likatafutiwa ufumbuzi kwa kuwatafuta wahusika na kuwasikiliza madai yao ili hatua za malipo ziendele kuchukuliwa.

Akizungumza na uongozi wa Wizara hiyo kupitia Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Nyumba pamoja na Uongozi wa Shirika hilo, Dk. Shein alisisitiza haja ya Shirika hilo kuzitambua na kuziorodhesha ili kujua idadi ya nyumba zao zote za Unguja na Pemba pamoja na zile za Wakala hatua ambayo pia, itasaidia kuepusha udanganyifu.

Dk. Shein alitumia fursa hiyo kutoa pongezi kwa Bodi ya Shirika hilo pamoja na uongozi wa Shirika hilo kwa  mafanikio makubwa yaliopatikana kwa kipindi kifupi.


Alieleza haja ya kuwepo utaratibu wa kuwatambua wakaazi wananoishi katika nyumba zote za Mji Mkongwe wa Zanzibar ili iwe rahisi katika kutekeleza mipango ya Serikali huku akieleza azma ya Serikali ya kujenga miji ya kisasa sambamba na kutekeleza mradi wa kufukia bahari katika eneo la pwani ya Gulioni kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za kisasa zikiwemo hoteli.

Wakati huo huo, Dk. Shein alikutana na uongozi wa Wizara hiyo walioongozana na Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Uhifadhi na Uendelezaji Mji Mkongwe na Uongozi wa Mamlaka ya Uhifadhi na Uendelezaji Mji Mkongwe na kueleza umuhimu wa kuweka utaratibu maalum juu ya kupunguza foleni ya gari katika barabara inayopita katika  Bandari ya Malindi.

Aidha, alieleza haja ya kuzingatia na kufuata kanuni na misingi ya Sheria iliyounda Bodi hiyo ili Mamlaka hiyo na Bodi yake iweze kufanya kazi kwa ufanisi pamoja na kufuata Sheria nyengine zote muhimu huku akieleza umuhimu wa uhifadhi wa mji huo.

Nae Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd alieleza kwamaba tabia ya kukodishwa nyumba kwa kutumia vilemba ambapo hatua hiyo ndio chanzo kikubwa cha upotevu wa nyumba za Serikali huku akisikitishwa na baadhi ya wananchi waliopewa nyumba na Serikali na wao kuzikodisha ama kuziuza bila ya kufuata taratibu na sheria zilizopo.

Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji Balozi Ali Karume kwa upande wake alieleza hatua zzinazoendelea kuchukuliwa katika Wizara yake katika kutoa ushirikiano uliopo kwa viongozi, wafanyakazi, Bodi pamoja na wajumbe wake.

Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi Abdulhamid Yahya Mzee kwa uonde wake alisisitiza haja ya kuimarisha usalama katika viwanja vya ndege vya Zanzibar kwani Mashirika ya ndege na hata wageni hilo wamekuwa wakilipa kipaumbele.

Mwenyekiti wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar Abdulhani Msoma aalieleza kuwa mapato yanayokusanywa katika viwanja vya ndege yameongezeka kutoka TZS Bilioni 12.9 mwaka 2011/2012 hadi kufikia TZS Bilioni 39.3 mwaka 2016/2017.

Alieleza kuwa idadi ya mashirika ya ndege imeongezeka kutoka mashirika 63 mwaka 2011 hadi mashirika 78 mwaka 2016 ambapo kati ya mashirika hayo, mashirika ya kimataifa yameongezeka kutoka 39 mwaka 2011 hadi 48 mwaka 2016 na mashirika 24 ya ndani yameongezeka hadi kufikia 30 mwaka 2016.

Aliongeza kuwa idadi ya abiria imeongezeka kutoka 753,971 mwaka 2011 hadi abiria 1,032,043 mwaka 2016 sawa na asilimia 137 kati ya abiria hao abiria wa kimataifa wameongezka hadi kufikia 529,696 mwaka 2016 kutoka abiria 283,755 mwaka 2011.   

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Zanzibar Mohamed Hafidh Rajab alisema kuwa licha ya uchanga wa Shirika hilo lakini ukusanyaji wa mapato yataongezeka kutoka TZS bilioni 1.6 mwaka 2017/2018 hadi kufikia TZS bilioni 48 katika mwaka 2021/2022 huku akieleza azma ya ujenzi wa nyumba za makaazi zikiwemo za wananchi wenye kipato cha chini.

Nao uongozi wa Mamlaka ya Uhifadhi na Uendelezaji Mji Mkongwe na Bodi yake ulieleza kuwa baadhi ya Mashirika ya Umoja wa Mataifa pamoja na washirika wa maendeleo wameonesha azma ya kuendelea kuiunga mkono Zanzibar katika kuuimarisha Mji Mkongwe wake ikiwa ni pamoja na kuzifanyia ukarabati mkubwa baadhi ya nyumba huku ukieleza hatua zilizofikiwa katika utekelezaji wa miradi yake.

Katika vikao vya leo, Dk. Shein alikutana na Uongizi wa Wizara hiyo pamoja na Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, uongozi wa Mamlaka pamoja na Bodi ya Shirika la Nyumba na Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Uhifadhi na Uendelezaji Mji Mkongwe na uongozi wake.

 Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.