Habari za Punde

Waziri wa Biashara Viwanda na Masoko Zanzibar Balozi Amina Salum Ali Azindua Baraza la Wazalishashi wa Bidhaa Za Viwandani Zanzibar.i

Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Viwanda na Wakulima Zanzibar ZNCCIA Toufiq Salim Turky akizungumza wakati wa Uzinduzi wa Baraza la Wazalishaji wa Bidhaa za Viwanja Zanzibar lililozinduliwa na Waziri wa Biashara Viwanda na Masoko Zanzibar Mhe Balozi Amina Salum Ali, uzinduzi huo umefanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Malindi Zanzibar na kuwashirikisha Wazalishaji wa Bidhaa za Viwandani Zanzibar. 
Baadhi ya Wafanyabishara ya Uzalishaji wa Viwandani Zanzibar wakifuatilia Uzinduzi huo wa Baraza la Uzalishaji Bidhaa Zanzibar katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Malindi Zanzibar.
Rais wa Jumuiya ya Wafanyabiashara ya Viwanda na Wakulima ZNCCIA Toufiq  Salim Turky akitowa changamoto zinazowakabili Wafanyabiashara Zanzibar wakati wa hafla hiyo ya Uzinduzi iliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Malindi Zanzibar.
Waziri wa Biashara Viwanda na Masoko Mhe Balozi Amina Salum Ali akihutubia na kuzindua Baraza la Uzalishaji wa Bidhaa Zanzibar katika ukumbi wa hoteli ya Golden Tulip Malindi Zanzibar na kutowa nasaha zake kwa wamiliki wa viwanja kuzalisha biashara zilizo bora kuweza kuingia katika Soko la Ushindani wa Bidhaa za Viwandani katika Soko la Afrika Mashariki na Kimataifa.
Waziri Balozi Amina Salum Ali akisisitiza jambo wakati akizungumza wakati wa uzinduzi huo kwa wamiliki wa viwanja Zanzibar.















No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.