Habari za Punde

Bodi ya Chakula Dawa na Vipodozi Yaangamiza Chakula Aina ya Soseji Zilizokwisha Muda Wake.

Wafanyakazi wa Bodi ya Chakula Dawa na Vipodozi wakiteremsha boksi za Chakula aina ya Soseji zilizokwisha muda wake kwa ajili ya kuangamizwa baada ya kugundulika katika Ghala la chakula linalomilikiwa na Kampuni ya Best Inmport Maruhubi na wakaguzi ,Kibele Wilaya ya Kusini Unguja.
Chakula aina ya Soseji zilizokwisha muda wake zikiwa zimekusanya kwa ajili ya kuangamizwa baada ya kugundulika katika Ghala la chakula linalomilikiwa na Kampuni ya Best Inmport Maruhubi na wakaguzi ,Kibele Wilaya ya Kusini Unguja
Mkuu wa kitengo cha Ufatiliaji madhara ya Chakula Aisha Suleiman akizungumza na Waandishi wa Habari katika zoezi la kuangamiza Chakula aina ya Soseji zilizokwisha muda wake na kwamba hazifai kutumiwa na maisha ya Binaadamu ,Kibele Wilaya ya Kusini Unguja.
Mkaguzi wa Chakula Bi Amina Ramadhan Salim akizungumza na Waandishi wa Habari katika zoezi la kuangamiza Chakula aina ya Soseji zilizokwisha muda wake na kwamba hazifai kutumiwa na maisha ya Binaadamu ,Kibele Wilaya ya Kusini Unguja.
Chakula aina ya Soseji zilizokwisha muda wake zikisangwa na baadae kufukiwa baada ya kugundulika kua hazifai kutumiwa na maisha ya Binaadamu ,Kibele Wilaya ya Kusini Unguja.
(Picha na Yussuf Simai Maelezo Zanzibar.)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.