Mh. Selemani Jafo, alipokuwa akifunga mafunzo ya siku tano kwa Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Mikoa minane kwenye ukumbi wa Hazina Mjini Dodoma.
Mh. Josephine Matiro Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga akitoa neon la Shukrani mara baada yakufungwa kwa mafunzo hayo.
Bibi Zainabu Chaula, Naibu Katibu Mkuu Afya TAMISEMI, alipokuwa akitoa neon kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kufunga Semina hiyo
Baadhi ya Wakurugenzi na Wakuu wa Wilaya wakisikiliza kwa makini Hotuba ya Ufungaji wa Semina hiyo ya siku tano. (Picha zote na Idara ya Habari Maelezo- Dodoma)
Na. Atley Kuni- TAMISEMI-
Dodoma.
Wakuu wa wilaya na
Wakurugenzi wa Mamlaka za serikali za Mitaa,
kutoka katika mikoa minane hapa nchini wame iahidi serikali ya awamu ya
tano inayo ongozwa na Mh. Dkt. John Pombe Magufuli makubwa mara baara yakumalizika kwa mafunzo
ya siku tano yaliyo endeshwa na Taasisi
ya Uongozi Institute kwa lengo
lakuwaimarisha watendaji hao wakuu katika ngazi ya Wilaya na Halmashauri katika
majukumu yao ya kila siku.
Akizungumza kwa niaba ya
wenzake Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mjini, Josephine Matiro, amesema mafunzo
hayo yaliyo washirikisha jumla ya washiriki 84 kati ya 89 waliokuwa wahudhurie
yamewakumbusha majukumu yao lakini kuwaongezea uzoefu kutokana na wao kutoka
maeneo tofauti tofauti.
“Tulivyo kuja sio tunavyo
ondoka, miongoni mwetu tulikuwa tunagombana katika maeneo yetu sisi na
wakurugenzi lakini kupitia semina hii, tunaondoka tukiwa tumepatana” alisema
Matiko na kuongeza,
“Mhe. Naibu Waziri sisi
tuahidi kwamba, tunakwenda kubadilika kwani mafunzo haya yamekuwa na manufaa
makubwa, labda tuombe jambo moja mafunzo haya yawe ya mara kwa mara, kwakuwa
yanasaidia hata kupungua Pressure na stress za kukaa kituoni kwa muda mrefu,
tunapokutana hivi inatusaidia kubadilishana uzoefu.
Mh.
Naibu waziri Selemani Jafo.
Akifunga mafunzo hayo,
Naibu Waziri wa Nchi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Mh. Selemani Jafo,
amewataka wakuu hao wa Wilaya na wakurugenzi, kuacha kuingiliana katika
utendaji badala yake wazingatie mipaka ya kazi inayo waongoza.
Mipaka
ya kazi.
“Waheshimiwa wakuu wa
Wilaya ninyi mpo kwaajili yakumwakilisha Mh. Rais katika maeneo yenu, hivyo
msifanye Interference badala yake mkafanye intrevession, Wataalam na mkurugenzi
wakisha amua kama mkuu wa Wilaya vema mkashauriana kwa hoja na kukubaliana kwa
misingi yakujenga na sio kubomoa.”
Kero
za Wananchi
Jafo amewataka Viongozi
hao kwenda kusimamia sheria, taratibu na kanuni bila ya kumuonea mtu, huku
akwasisitiza kwenda kujenga nidhamu na kutatua kero za wananchi ili kero zinazo
fikishwa ngazi ya Wizara zikomee huko huko kwakuwa katika ngazi ya Wilaya na
Halmashauri wapo wataalam wengi hivyo ametaka wataalam hao watumike vema.
“Matatizo yatakayo washinda basi vema mkayafikisha katika Ngazi ya mkoa, sio
kuwaacha wananchi wanalipa nauli zao kupeleka kero Wizarani” Mh.Jafo
Vita
ya Dawa zakulevya na Rushwa
Naibu waziri Jafo hakuacha
kuwahimiza viongozi hao kwenda kupambana na dawa za kulevya katika maeneo yao,
“Kapambaneni na vita dhidi ya dawa za kulevya, tunafahamu dawa zakulevya imekuwa
mwiba mchungu kwa nguvu kazi ya Taifa, tukailinde nguvu kazi hii na agenda hii
iwe ya kudumu katika vikao vyenu vyote vya maamuzi”, “Aidha adui Rushwa
msimuache akastawi katika maeneo yenu, haiwezekani mgonjwa akakosa bomba la
sindano.
Makusanyo
kwa njia ya kieletroniki
Naibu Waziri Selemani Jafo
amewaagiza wakurugenzi kukusanya mapato kwa njia ya mifumo ya kieletroniki na
kuonya wale wote wanaofanya diversion ya mifumo iliwarudi kwenye njia za
kizamani, “Jiji la Dar es Salaam leo, nimpongeze sana dada yangu Zipolla,
amekuwa mfano wa kuigwa kutoka Mil. 15 hadi Mil 600 ya makusanyo ya ushuri wa
maegesho ambapo hapo awali wengine walishindwa hii ni hatua yakupigiwa mfano,
ajenda ya mapato iwe yetu sote.”
Usimamizi
wa Rasilimali na thamani ya fedha.
“Lazima (value for Money)
katika miradi yetu yote mkaipe kipaumbele, jana nimetoa Press na maelekezo
yamekwenda tayari juu ya ukarabati wa Vituo 172 vya afya nchini kote kwakuwa
fedha hizo nimeelekeza mtumie force Account, niseme ule msemo wa vijana wa mtaani, {Kipa
katoka}, kazi kwenu lakini ifikapo
Desemba 30, 2017 kazi hiyo iwe imekamilika alisema Jafo na kuongeza kuwa,
“Tulifanya vema katika shule kwenye zile Bil 25 leo watoto wote wapo shule,
tukafanye vizuri pia katika hili la Vituo vya afya”.
Mwisho Naibu Waziri Jafo
hakuacha kuwaonya Viongozi hao dhidi ya matumizi mabaya ya sheria inayowaruhusu kuamuru kumuweka mtu
rumande kwa saa 48, “sheria hii ipo lakini itumike kunapo sababu sio kuitumia
kiholela” alisema Mh. Jafo.
Salaam
za Uongozi Institute
Akitoa salaama za Uongozi
institute Mkuu wa kitengo cha mafunzo
Kadai Singo, alisema mambo makubwa wanayotazamia mara baada ya mafunzo
hayo ni pamoja na Weledi, Mbadiliko, Wilaya zibadilike lakini kupata mrejesho
wa matokeo chanya baada ya mafunzo kukamilika.
Salaam
za TAMISEMI na Dkt. Zainabu Chaula
Awali akitoa taarifa fupi
juu ya mwenendo wa mafunzo kabla yakumkaribisha Mh. Naibu Waziri kufunga
mafunzo hayo Naibu Katibu Mkuu Afya Dkt. Zainabu Chaula alisema, “Mara baada
yakukamilika kwa mafunzo hayo yaha shabaha ya Wizara ni kuwapatia mafunzo ya
aina hii Wah. Wakuu wa Mikoa ili katika utendaji wakawe na uelewa wa pamoja”,
Dkt. Chaula alimueleza Naibu Waziri aliyefika kufunga mafunzo hayo.
Mikoa ambayo wakuu
Wawilaya ambao wamepatiwa mafunzo hayo katika awamu hii ilikuwa ni Shinyanga, Mbeya, Rukwa, na Ruvuma, Mikoa
mingine ni Songwe, Dar es Salaam, Njombe
na Iringa.
No comments:
Post a Comment