Na Ali Othman Ali, Pemba
Afisa Mdhamini Wizara ya Habari Utalii
Utamaduni na Michezo Mh. Khatibu Juma Mjaja ameelezea matumaini yake ya mafanikio katika sekta ya
utalii kisiwani Pemba kupitia tamasha la michezo na utamaduni lililoandaliwa na
Taasisi ya Rafiki Network.
Akizungumza mara baada ya kupokea cheti cha
shukrani Ofisisni kwake Chake Chake Bwana Mjaja amesema Rafiki Network
imefungua njia katika kuimarisha utalii wa ndani na nje ya nchi kutokana na
kuandaa na kusimamia Tamasha la kimichezo liloandaliwa kwa ubunifu na ustadi
huku likijumuisha michezo mbali mbali ya asili ambayo niburudani kwa wenyeji na
kivutio kwa wageni.
Mh. Mjaja ameuomba uongozi wa Taasisi ya
Rafiki Network kuhakikisha kwamba Tamasha hili linakua endelevu ambapo
amebainisha kwamba kuendelea kwa tamasha hilo kila mwaka kutasaidia kukuza hali
za watu katika Nyanja mbali mbali kiuchu na kiutamaduni.
Akifafanua ubunifu uliofanyika katika
maandalizi ya Tamasha la kimichezo Kisiswani Pemba, Mh. Mjaja amesifu uteuzi na
mpangilio wa barabara zilizotumika katika mchezo wa mbio za Baiskeli nakuongeza
kwamba mpangilio huo uliwapa fursa wananchi waliowengi kuweza kushiriki
kikamilifu katika michezo mbali mbali. Afisa huyo pia amewapongeza Azam TV kwa
kurusha matangazo ya moja kwa moja ya Bonanza hilo.
Nae Afisa Mdhamini Kamisheni ya Utalii
Pemba Maalim Suleiman Amour Suleiman amepokea Cheti cha Shukrani kutoka kwa
Taasisi ya Rafiki Network kutokana na mchango wake mkubwa katika kufanikisha
Tamasha hilo.
Taasisi ya Rafiki Network iliandaa Tamasha
la kimichezo Kisiwani Pemba mnamo Julai 28-30 ambalo lilijumuisha michezo mbali
mbali ikiwa ni pamoja na mchezo wa Ng’ombe, Mashindano ya Baiskeli, Mashindano
ya kuogelea na Resi za Ngalawa.
No comments:
Post a Comment