Kamishna
Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Nchini – Thobias Andengenye, ataongoza
Maafisa na Askari katika zoezi la kuuaga mwili wa Marehemu na kutoa heshima za
mwisho (Kwa Paredi Maalum), kwa aliyekuwa Kamishna Mstaafu wa Operesheni wa
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji CF (OPS) Rogatius Peter Kipali, ambaye alifariki dunia
Semptemba 7, 2017 akiwa nyumbani kwake Mombasa, Ukonga Jijini Dar es Salaam.
Zoezi
la kuuaga mwili wa Marehemu litafanyika kesho Semptemba 10, 2017 kuanzia saa
3:00 asubuhi katika viwanja vya Kituo cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa
Ilala eneo la (FIRE) Jijini Dar es
Salaam.
Kamishna
Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji anapenda kuvitaarifu Vyombo vya Ulinzi
na Usalama, Maafisa, Askari na Watumishi wote wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,
, familia ya Marehemu na wale wote walioguswa na msiba huu kwa namna moja au
nyingine kujitokeza kwa ajili ya kutoa heshima zao za mwisho.
IFUATAYO NI RATIBA NZIMA YA MSIBA
Bwana alitoa
na bwana ametwaa, jina la bwana lihimidiwe
Amina.
IMEANDALIWA NA KITENGO CHA HABARI NA
ELIMU KWA UMMA-JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI
No comments:
Post a Comment