Habari za Punde

TANZIA: KAMISHNA MSTAAFU WA OPERESHENI WA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI KUAGWA KESHO JIJINI DAR ES SALAAM.

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Nchini – Thobias Andengenye, ataongoza Maafisa na Askari katika zoezi la kuuaga mwili wa Marehemu na kutoa heshima za mwisho (Kwa Paredi Maalum), kwa aliyekuwa Kamishna Mstaafu wa Operesheni wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji CF (OPS) Rogatius Peter Kipali, ambaye alifariki dunia Semptemba 7, 2017 akiwa nyumbani kwake Mombasa, Ukonga Jijini Dar es Salaam.

Zoezi la kuuaga mwili wa Marehemu litafanyika kesho Semptemba 10, 2017 kuanzia saa 3:00 asubuhi katika viwanja vya Kituo cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Ilala eneo la (FIRE) Jijini Dar es Salaam.

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji anapenda kuvitaarifu Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Maafisa, Askari na Watumishi wote wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, , familia ya Marehemu na wale wote walioguswa na msiba huu kwa namna moja au nyingine kujitokeza kwa ajili ya kutoa heshima zao za mwisho.

IFUATAYO NI RATIBA NZIMA YA MSIBA

Bwana alitoa na bwana ametwaa, jina la bwana lihimidiwe
     Amina.


IMEANDALIWA NA KITENGO CHA HABARI NA ELIMU KWA UMMA-JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.