Habari za Punde

SMZ: Serikali inaendelea kuungwa mkono na mataifa ya kigeni duniani

  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Issa Gavu (kulia) akizungumza na waandishi wa vyombo vya habari kuhusu tathimini ya ziara ya Ujumbe wa Mfalme wa Oman, Qaboos bin Said Al-Said uliozuru Zanzibar hivi karibuni. Kushoto ni Mshauri wa Rais wa Zanzibar katika masuala ya Ushirkiano wa Kimataifa, Fedha na Uchumi Mohamed Abdiwawa.


  Baadhi ya Waandishi wa vyombo vya habari wakifuatilia mkutano wa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Issa Gavu (kulia) akizungumza na waandishi wa vyombo vya habari kuhusu tathimini ya ziara ya Ujumbe wa Mfalme wa Oman, Qaboos bin Said Al-Said uliozuru Zanzibar hivi karibuni.
 Baadhi ya Waandishi wa vyombo vya habari wakifuatilia mkutano wa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Issa Gavu (kulia) akizungumza na waandishi wa vyombo vya habari kuhusu tathimini ya ziara ya Ujumbe wa Mfalme wa Oman, Qaboos bin Said Al-Said uliozuru Zanzibar hivi karibuni. 

 Baadhi ya Waandishi wa vyombo vya habari wakifuatilia mkutano wa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Issa Gavu (kulia) akizungumza na waandishi wa vyombo vya habari kuhusu tathimini ya ziara ya Ujumbe wa Mfalme wa Oman, Qaboos bin Said Al-Said uliozuru Zanzibar hivi karibuni.

Na Ismail Ngayonga MAELEZO


SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar imetoa hofu wananchi na kuwaeleza kuwa mataifa mbalimbali duniani yanaendelea kuunga mkono na kutoa ushirikiano mkubwa kwa Rais Dkt. Ali Mohamed Shein katika jitihada mbalimbali zake za kuwalelea maendeleo Wazanzibar.

Hayo yamesemwa leo (Jumamosi Oktoba 21, 2017) Mjini Zanzibar na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Issa Gavu wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu tathimni ya ziara ujumbe wa Mfalme wa Oman, Qaboos bin Said Al-Said aliyetembelea Zanzibar tarehe 22 Septemba mwaka huu.

Gavu alisema katika kudhihirisha kuimarika kwa uhusiano na mataifa mbalimbali duniani, Serikali ya Zanzbar tayari imepokea mialiko tisa ya ziara za nje ya nchi zinazotarajiwa kufanywa na Rais Dkt. Ali Mohamed Shein na Viongozi wa 
Serikali kuanzia mwishoni mwa mwezi Januari 2018.

“Serikali inaendelea kupanua wigo wa ushirikiano wa kidiplomasia na mataifa ya kigeni, hakuna haja ya wananchi kuwa na hofu, na tutaendelea kukaribisha ushirikiano na mataifa ya nchi jirani kwa ajili ya kuharakisha maendeleo ya wananchi wetu” alisema Gavu

Gavu alisema tangu kuingia madarakani kwa Rais Shein, Novemba 2015 uhusiano wa Zanzibar na mataifa mbalimbali ulimwengu umekuwa ukiimarika na kueleza kuwa Kiongozi tayari amesafiri katika mataifa ya Djibout, Morroco na Commoro.

Aidha Gavu alisema katika kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia na nchi marafiki, nchi ya Saudi Arabia inatarajia kufungua Ofisi ndogo ya Ubalozi Zanzibar na hivyo kuwataka Wananchi wa Zanzibar kuendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali yao ikiwemo kudumisha amani, umoja na mshikamano.

Akizungumzia kuhusu ziara ya Mfalme Qaboos bin Said Al-Said wa Oman aliyoifanya Zanzibar hivi karibuni, Serikali ya Zanzibar tayari imeunda timu ya wataalamu kwa ajili ya kufuatilia utekelezaji wa makubaliano yaliyofikiwa baina ya mfalme wa Oman na Rais Shein.

Aliongeza kuwa katika ziara hiyo, Mfalme wa Oman alikubali kutoa ufadhili wa mafunzo ya muda mfupi na mrefu kwa wanafunzi wa wanafunzi wa Zanzibar katika masuala ya mafuta na gesi pamoja na kujenga viwanda vya kusindika samaki.

“Tutahakikisha kuwa tunapeleka vijana wenye sifa na weledi katika masomo hayo ili kuhakikisha kuwa Zanzibar inatumia vyema fursa hiyo, ambapo kwa kuanzia hivi sasa wapo wanafunzi wa masomo hayo katika nchi ya China wakipata ujuzi wa tasnia ya mafuta” alisema Gavu.

Wakati wa ziara ya ujumbe wa Oman, Waziri Gavu alieleza kuwa katika mazungumzo ya ya ujumbe huo na Rais Shein, Mfalme Qaboos bin Said Al-Said alikubali pia kufanya matengenezo makubwa ya jengo la Beit –el Ajab pamoja na jengo la “People’s palace”, hatua inayolenga kuimarisha ukuaji wa sekta ya utalii Zanzibar.

Kwa upande wake Mshauri wa Rais wa Zanzibar katika masuaala ya Ushirikiano wa Kimataifa, Fedha na Uchumi, Balozi Mohamed Ramia Abdiwawa aliwataka Wazanzibar kuungana pamoja na kuendelea kumuunga mkono Rais Ali Mohamed Shein hususani katika jitihada zake za kuimarisha ushirikiano na mataifa ya kigeni.

Balozi Ramia alisema katika siku za hivi karibuni kumeibuka hofu isiyo na sababu kuhusu ziara ya Mfalme Qaboos Said Al-Said na kueleza kuwa katika mazungumzo baina ya Viongozi hao wawili hakukuwa na suala la kisiasa lililojadiliwa badala yake ni masuala ya uimarishaji wa ushirikiano wa maendeleo ya wananchi.


“Kuna minong’ono kuwa Zanzibar ilibanwa na mfalme Qaboos Said Al-Said kuhusu hali ya kisiasa, jambo hilo hakuna na badala yake Viongozi ho walijadili masuala ya ushirikiano na hatua zinazopaswa kuchuliwa ili kuharakisha maendeleo ya wananchi wa pande zote mbili”

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.