Habari za Punde

TACOSODE Watoa Dira ya Kutatua Changamoto za Sekta ya Afya Hasa Vijijini.

Mkurugenzi wa Miradi wa Tacosode, Theofrida Kapinga akizungumza jambo wakati wa semina iliyofanyika katika ukumbi wa valentine mkoani Iringa
Afisa mchechemzi wa mradi Abrahm Kimuli akiendelea kutoa elimu kwa wanasemina walikuwa wamehudhuria katika ukumbi wa valentine
Baadhi ya washiriki wakiwa kwenye mijadala ya sekta ya afya na jinsi gani wanaweza kutatua changamoto zinazoweza kuikoa sekta ya afya hapa nchini.


Na Fredy Mgunda,Iringa.
BARAZA la Vyama vya hiari na Maendeleo ya Jamii (TACOSODE) limesema wananchi wamekuwa na uelewa kuhamasisha bajeti kuwa na kipaumbele kwa changamoto zinazowakabili.

Hayo ameyasema Mkurugenzi wa Miradi wa Tacosode, Theofrida Kapinga wakati akizungumza semina ya kujadilia jinsi gani ya kutatua changamoto zinazoikumba sekta ya afya iliyofanyika katika ukumbu wa valentine Manispaa ya Iringa.

“Unajua zamani wananchi hata viongozi wa sekta ya afya walikuwa wagumu kuelezea changamoto zinazowakabili lakini saizi wananchi na viongozi wamekuwa na elimu ya kutosha juu ya kueleza changamoto zilizopo katika sekta hiyo ndio maana vitu vingi vinaibuka muda huu” alisema Kapinga

Kapinga alisema licha ya serikali kufanya juhudi kutatua changamoto ili kuto huduma ya afya bora lakini bado sekta hiyo inaendelea kukabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo zinakwamisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wananchi.

“Ukiangalia tafiti nyingi zinaonyesha kuwa serikali imekuwa ikishindwa kuongeza bajeti ya sekta ya afya ili kufikia asilimia 15 ya bajeti yote ya serikali kwa kuzingatia azimio la Abuja” alisema Kapinga

Aidha kapinga alisema kuwa moja ya changamoto kubwa ni uhaba wa kupatikana kwa dawa muhimu,vitendanish na vifaa tiba kulinganisha na utafiti wa mwaka 2012 ulifanywa na taasisi ya afya ya Ifakarana kugundua kuwa asilimia 41 ya dawa muhimu zinahitajika kwa kiasi kikubwa.

Kwa upande wake afisa mchechemzi wa mradi Abrahm Kimuli aliwataka watumishi wa sekta ya afya kuzibaini changamoto zinazowakabili na kuzitafutia ufumbuzi kushirikiana na serikali panoja na sekta binafsi.

“Unajua kweli kuna changamoto nyingi ambazo zinawakabili hivyo ni lazima muwe wabunifu kuzitafutia ufumbuzi lakini kwenye hizi sekta binafsi kuwa wasomi wengi ambao wanaweza kutoa ushauri mzuri wa kutatua changamoto zilizopo” alisema Kimuli 

Kimuli alisema kuwa wananchi wamekuwa na uelewa wa maswala ya afya kutokana na elimu waliopata katika mradi wa uhamasishaji wananchi kushiriki katika masuala ya afya katika kuangalia vipaumbele vya bajeti uliokuwa ukitekelezwa katika Mikoa ya Iringa pamoja na Dodoma.

Alisema kuwa wananchi mradi huo katika utekezwaji wake katika Halmashauri ya Iringa pamoja na Kongwa mkoani Dodoma wananchi wamekuwa na mwamko katika masuala ya afya ushiriki kwa kuchangia katika huduma za afya.

Kimuli alisema kuwa mradi huo wa miaka minne umekuwa na matokeo katika wilaya ambazo umetekelezwa kwa wananchi kuwa na mwamko katika masuala ya huduma za afya kwa kuchangia hata nguvu zao pale panapobidi.

Aidha amesema kuwa mradi huo ukiisha wanaweza kufanya katika sekta zingine ili kuwa maendeleo ya katika masuala mbalimbali kutatuliwa.

Akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Iringa Abel Mgimwa alisema kuwa serikali ya awamu ya tano imejipanga kuahakikisha changamoto zinatatuliwa kimkakati kulinga na bajeti wanayokuwa wameipanga.

“Ukiangalia bajeti ya mwaka wa fedha mwaka huu imepanda hivyo ni dalili njema za kuanza kutatua changamoto ambazo zimekuwa zikidumu kwa miaka mingi na kuwaomba wananchi na viongozi kuwa na subira katika kipindi hiki cha utatuzi wa changamoto hizo” alisema Mgimwa

Mgimwa aliwapongeza TACOSODE kwa mchango wao katika sekta ya afya ambayo imekuwa na changamoto nyingi hivyo sio rahisi kwa serikali kutatua kwa haraka hivyo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.