Mkurugenzi
wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania Bi. Beatrice Singano (kulia) akizungumza na
Waandishi wa Habari na Maafisa wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, katika
makabidhiano ya msaada wa simu zitakazotumika kwenye namba ya dharura 114
yaliyofanyika Makao Makuu ya Jeshi, jijini Dar es Salaam
Kamishna
Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye (katikati),
akipokea msaada wa simu kutoka kwa Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Aitel Tanzania
Bi. Beatrice Singano (kushoto), katika makabidhiano ya msaada wa simu
zitakazotumika kwenye namba ya dharura 114 yaliyofanyika Makao Makuu ya Jeshi, jijini
Dar es Salaam
Kamishna
wa Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye (kushoto)
akizungumza na Waandishi wa Habari, Maafisa wa Zimamoto na Uokoaji na
Wafanyakazi wa Airtel, katika makabidhiano ya msaada wa simu zitakazotumika
kwenye namba ya dharura 114 yaliyofanyika Makao Makuu ya Jeshi, jijini Dar es
Salaam
Kamishna
Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye (Kulia), Kamishna
wa Operesheni Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Billy Mwakatage (kushoto) na Mkurugenzi
wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania Beatrice Singano (katikati) wakishika
kipeperushi kinachoonyesha namba ya dharura 114 ya Jeshi. katika makabidhiano ya msaada wa simu
zitakazotumika kwenye namba ya dharura 114 yaliyofanyika Makao Makuu ya Jeshi, jijini
Dar es Salaam
Picha ya Pamoja, Kamishna
Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye (wa pili kulia)
akiwa na Maafisa waandamizi wa Jeshi hilo pamoja na Mkurugenzi wa Mawasiliano
wa Airtel Tanzania Bi. Beatrice Singano (wa tatu kulia), katika makabidhiano ya
msaada wa simu zitakazotumika kwenye namba ya dharura 114 yaliyofanyika Makao
Makuu ya Jeshi, jijini Dar es Salaam leo (Picha na Jeshi la Zimamoto Na Uokoaji)
IMEANDALIWA
NA KITENGO CHA HABARI NA ELIMU KWA UMMA - JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI
Airtel Tanzania imetoa
msaada wa simu kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ambazo zitatumika kwa ajili ya
kurahisisha na kuimarisha mawasiliano ya namba ya dharura 114 wakati wa kutoa
taarifa za dharura za moto na majanga mbalimbali nchini.
Simu hizo zimetolewa
kwa Mikoa yote ya Jeshi la Zimamoto ambapo wateja wa Airtel watapiga bure
ilikupata huduma za Jeshi hilo.
Akikabidhi simu hizo,
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania Beatrice Singano alisema wao kama
Airtel wanatambua umuhimu wa Jeshi hilo na wanaamini kuwa wananchi sasa
wataweza kupata huduma za Jeshi hilo kwa urahisi kupitia namba hiyo ya dharura.
“Airtel tunatambua umuhimu wa Jeshi la
Zimamoto na Uokoaji katika jamii, hivyo tunaamini utoaji wa taarifa za majanga
kwa wakati muafaka unarahisisha shughuli za uokoaji na kuzuia kwa kiwango
kikubwa hasara ambayo inaweza kusababishwa na majanga hayo katika jamii”
alisema Mkurugenzi huyo.
Kwa Upande wake Kamishna
Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Nchini, Thobias Andengenye aliishukuru
Kampuni ya Airtel kupitia Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania Beatrice Singano kwa msaada huo wa simu
na kusema utaimarisha utendaji wa Jeshi hilo.
Wateja wa Airtel sasa
wataweza kupata huduma kwa haraka baada ya kupiga simu. “Tunashukuru sana na
tuna imani kuwa wateja wa Airtel sasa watakuwa na urahisi wa kutufikia kupitia
namba 114, tofauti na hapo nyuma”
alisema Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo
Natoa rai kwa wananchi kuendelea kutumia vema
mitandao ya simu kwa kutolea taarifa za kweli na si vinginevyo, hatua kali za
kisheria zitachukuliwa kwa mwananchi yeyote atakayetumia vibaya mawasiliano ya
kimtandao, hasa kwa kuitumia vibaya namba ya dharura 114 inayotumiwa na wananchi kutolea taarifa za matukio ya moto,
maokozi na majanga mengine.
No comments:
Post a Comment