Habari za Punde

Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar Afanya Ziara Ofisi za Uhamiaji Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari Masoud Sururu (kati kati), akiwatoa hofu Watendaji wa Mamalaka ya Vitambulisho vya TAifa (NIDA) kwamba kuanzia mwezi January 2018, Idara ya Uhamiaji Zanzbar imejipanga kushughulikia maombi ya Vitambulisho vya Taifa kwa Raia wote watakaofika katika Ofisi yao iliyopo Kinduni, Wilaya ya Kaskazini “B” Unguja, badala ya kufuata huduma Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Kaskazini iliyopo Kivunge. Hatua hiyo ni utekelezaji wa Ahadi za Serikali kufikisha huduma karibu na Wananchi. Aliyasema hayo wakati alipotembelea Ofisi hizo wakati wa ziara ya kikazi katika Wilayani humo tarehe 05  - 06 Disemba, 2017.  

Sheha wa Shehia ya Kiwengwa Bwana Maulid Masoud Ame, akimuleza Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari Masoud Sururu na Maafisa waandamizi wa Idara hiyo alioambatana, changamoto za wageni katika maeneo yao. Wakat wa ziara ya kikazi kujionea utendaji kazi wa Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Kaskazini Unguja na Wilaya zake tarehe 05 - 06 Disemba, 2017.
Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari Masoud Sururu (kati kati), akielezea jinsi Idara ya Uhamiaji inavyopiga hatua katika kutatua changamoto ya ufinyu wa Ofisi na Vitendea kazi katika Wilaya zote Unguja na Pemba, ambapo alisema hivi karibuni Idara yake inatarajia kupokea magari (12) na Pikipiki (20) ambazo kwa kiasi kikubwa zitakidhi uhaba uliopo. Aliyasema hayo wakati wa ziara ya kikazi kwenye maeneo mbali mbali Mkoa wa Kaskazini Unguja tarehe 05 - 06 Disemba, 2017. 
Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari Masoud Sururu, akiambatana na Maafisa Waandamizi wa Uhamiaji wakitembelea maeneo mbalimbali yanayotumiwa na Wahamiaji wasiofata Sheria katika ukanda wa Pwani za Kiwengwa, Pwani mchangani, Matemwe, Pongwe, Kendwa na Nungwi, wakati alipofanya  ziara ya kikazi katika maeneo yote yanayofanyiwa kazi na Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Kaskazini Unguja tarehe 05 - 06 Disemba, 2017.


Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji, Haroub Iddi Juma, akitoa ufafanuzi kwa Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari Masoud Sururu juu ya Ramani ya Kiwanja kilichopo kijiji cha Gamba, Wilayani ya Kaskazini “B” wakati alipotembelea kiwanja hicho jana tarehe 05 Disemba, 2017 kinachotarajiwa kujengwa Ofisi ya Uhamiaji Wilayani humo. 
Sheha wa Shehia ya Moga Bwana Juma Kombo Juma (kati kati), akimuonesha Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari Masoud Sururu mipaka ya Kiwanja kilichopo Shehia ya Gamba, Wilaya ya Kaskazini “B” kinachomilikiwa na Idara ya Uhamiaji. Hizo ni juhudi za Idara hiyo kufikisha huduma zake karibu na wananchi kwa kujenga Ofisi na Makaazi ya Askari katika Ofisi za Mikoa na Wilaya zote zilizopo Zanzibar.  

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.