Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, Atembelea Mradi wa Kiwanda Turkey Petrolium Cha Gesi Bumbwini Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Wafanyakazi wa Kampuni ya Turkey Petrolium, akiwa katika ziara yake kutembelea Kiwanda cha Gesi na Ujenzi wa Matenki ya kuhifadhia Gesi na Mafuta ya Kampuni hiyo huko Bumbwini Mkoa wa Kaskazini Unguja. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya VIGOR Tofiq Salim Turky, michezo ya eneo la Kiwanda cha Gesi na ujenzi wa Matenki ya Kuhifadhia Mafuta na Gesi Asili katika eneo hilo la Mradi Bumbwini Mkoa wa Kaskazini Unguja. alipofanya ziara kutembelea maeneo hayo.
Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya VIGOR Tofiq Salim Turkey akitowa maelezo ya ujenzi wa Mradi wa Matenki ya kuhifadhia Mafuta na Gesi Asili kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, alipofanya ziara kutembelea maeneo hayo hivi karibuni.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi na Viongozi wa Serikali wakiwa katika ziara ya kutembelea eneo lililotengwa kwa ajili ya Ujenzi wa Kituo cha kuhifadhia Mafuta ya Petrol katika eneo la mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja.



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.