Habari za Punde

Wajumbe wa Kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi wajionea majengo ya skuli yaliyoathirika na mvua

 JENGO la Skuli ya Madungu Sekondari Pemba, ambalo lilijengwa kwa msaada wa fedha za Benk ya Dunia na kufunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Mhe:Dk Ali Mohamed Shein, Januari mwaka 2013 jengo hilo kwa sasa limekuwa linavuja kipindi cha mvua huku wanafunzi wakishindwa kusoma.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 WAJUMBE wa Kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, wakiwa na viongozi wa Wizara ya Elimu Zanzibar, wakiwasikiliza wanafunzi waliomo ndani ya moja ya madarasa yanayovuja kipindi cha mvua, huku wanafunzi wakishindwa kusoma wakati wajumbe hao waliotembelea skuli hiyo na kujionea athari zilizopo.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 WAJUMBE wa Kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, wakiangalia juu katika moja ya madarasa pamoja na watendaji wa Wizara ya Elimu Zanzibar, wakiongozwa na ktibu mkuu wa Wizara hiyo Khadija Bakari Juma, wakati wajumbe hao walipotembelea skuli hiyo na kuangalia athari zilizopo.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 MJUMBE wa kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar na Mwakilishi wa jimbo la Tunguu, Mhe:Simai Mohamed Said, akimuuliza jambo katibu mkuu Wizara ya ELimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Khadija Bakari Waziri wakati alipotembelea skuli ya Madungu Sekondari na kujionea athari zilizopatikana kutokana na skuli hiyo kuvuja kipindi cha Mvua.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 MOJA ya sehemu ya juu ya darasa la skuli ya Madungu Sekondari, ikiwa imeharibika baada ya sehemu ya paa la skuli hiyo kuvuja katika kipindi cha mvua, maji kuharibu silingbord yote ya darasa hilo kama linavyoonekana katika picha.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 MAKAMU mwenyekiti wa kamati ya bajeti ya baraza la Wawakilishi Zanzibar, mwakilishi wa jimbo la Chambani Bahati Khamis Kombo akiongoza kikao cha wajumbe wa kamati yake na viongozi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, huko katika ukumbi wa skuli ya Madungu Sekondari Mjini Chake Chake.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

 WAJUMBE wa kamati ya bajeti ya baraza la Wawakilishi Zanzibar, wakitoka kukagua skuli ya Dk Omar Ali Juma Wawi Chake Chake Pemba, ikiwa ni moja ya skuli zilizoathiriwa na mvua kubwa ilionyesha Zanzibar.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Khadija Bakari Juma akisoma taafira ya mradi wa ZABEIP, kwa wajumbe wa kamati ya bajeti ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, wakati walipotembelea jengo la skuli ya Madungu Sekondari Chake Chake Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.