STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 24.02.2018
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali
Mohamed Shein amemtumia salamu za pongezi Kiongozi wa Taifa la Kuwait, Sheikh
Sabah Ahmad Al-Sabah kwa kuadhimisha miaka 57 ya siku ya uhuru wa Taifa hilo.
Salamu hizo zilieleza
kuwa wananchi wa Zanzibar wanaungana na ndugu zao wa Kuwait katika kusherehekea
siku hii adhimu kwa Taifa hilo.
Aidha, katika salamu hizo,
Dk. Shein alimuhakikishia Sheikh Sabah Ahmad Al-Sabah kuwa Zanzibar itaendeleza
uhusiano na ushirikiano uliopo kati yake na Kuwait.
Dk. Shein alimtakia
kiongozi huyo na familia yake pamoja na wananchi wote wa Kuwait afya njema na
sherehe njema katika kuadhimisha siku hiyo ya Taifa sambamba na kumtakia mafanikio
zaidi katika kuendelea kuipatia maendeleo zaidi ya kiuchumi nchi hiyo kwa
madhumuni ya kulinufaisha Taifa hilo na wananchi wake.
Kuwait inasherehekea siku
yake ya Taifa kila ifikapo Februari 25 ya kila mwaka ambapo nchi hiyo ilipata
uhuru wake kutoka kwa Wakoloni wa Kiengereza mnamo mwaka 1961 chini ya Jemedari
wa Taifa hilo Marehemu Sheikh Abdallah Al-Salem Al-Sabah aliyefariki dunia mnamo
mwaka 1965.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address:
2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment