Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia katika Mkutano huo
Maalum wa Wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) unaofanyika
Kampala nchini Uganda.
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Rais wa
Kenya Uhuru Kenyatta wakati wakielekea kwenye ukumbi wa Mkutano Maalum wa Wakuu
wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC unaojadili masuala mbalimbali
ikiwemo Maendeleo ya Sekta ya Miundombinu na Afya.
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amesimama pamoja na Mwenyekiti
wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais wa Uganda Yoweri Museveni wa nne kutoka
kulia, Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta pamoja na Rais wa Sudani ya Kusini Salva Kiir
wakati Wimbo wa Jumuiya ya Afrika
Mashariki ulipokuwa ukipigwa katika ukumbi wa mkutano uliopo katika eneo la Munyonyo Kampala nchini Uganda.
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amekaa pamoja na Mwenyekiti
wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais wa Uganda Yoweri Museveni wanne kutoka
kulia, Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta pamoja na Rais wa Sudani ya Kusini Salva Kiir
wakati wa mkutano huo Maalumu wa Wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki
unao endelea jijini Kampala.
Mwenyekiti wa
Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais wa Uganda Yoweri Museveni akifungua Mkutano
huo maalum wa Wakuu wa nchi za Jumuiya ya
Afrika Mashariki Kampala nchini Uganda.
Mwenyekiti wa
Jumuiya ya Afrika Mashariki Rais wa Uganda Yoweri Museveni katika picha na Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wa kwanza kulia,
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, pamoja na Rais wa Sudan ya Kusini Salva Kiir mara
baada ya Mkutano Maalum wa 19 wa Jumuiya
hiyo uliofanyika Kampala nchini Uganda.
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais wa Sudan ya
Kusini Salva Kiir kabla ya kuanza kwa mkutano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais wa Kenya
Uhuru Kenyatta kabla ya kuanza kwa mkutano huo wa 19 wa Jumuiya ya Afrika
Mashariki jijini Kampala Uganda.
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta mara baada ya
kupiga picha ya pamoja katika eneo la Munyonyo Kampala nchini Uganda. PICHA NA IKULU
No comments:
Post a Comment