Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akisalimiana na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji (R) Semistocles Kaijage akiwa na ujumbe aliofuatana nao walipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo (katikati) Makamu Mwenyekiti wa Tume hiyo Mhe.Hamid M.Mahmoud
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akimsikiliza Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji (R) Semistocles Kaijage (wa pili kulia) alipokuwa akiwatambulisha Viongozi aliofuatana nao walipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo kwa mazungumzo na Rais (katikati) Makamu Mwenyekiti wa Tume hiyo Mhe.Hamid M.Mahmoud
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji (R) Semistocles Kaijage alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo pamoja na ujumbe aliofuatana nao
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akifuatana na mgeni wake Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji (R) Semistocles Kaijage alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo pamoja na ujumbe aliofuatana nao
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akifurahia jambo alipokuwa akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji (R) Semistocles Kaijage (kushoto)wakiwepo na Viongozi wengine baada ya mazungumzo yao walipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo,[Picha na Ikulu.] 28/02/2018.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein amekutana na uongozi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na
kusisitiza haja ya kuendeleza umoja na mashirikiano yaliopo kati ya Tume hiyo
na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) ili Tanzania iendelee kupata heshima
ndani na nje ya Bara la Afrika.
Rais Dk. Shein
aliyasema hayo leo alipokutana na kufanya mazungumzo na uongozi wa Tume ya
Taifa ya Uchaguzi (NEC), Ikulu mjini Zanzibar ulipofika kwa ajili ya
kujitambulisha ukiongozwa na Jaji Semistocles Kaijage Mwenyekiti wa Tume hiyo
akifuatana na Makamu Mwenyekiti Jaji Mkuu Mstaafu wa Zanzibar Hamid Mahmoud
Hamid pamoja na Mkurugenzi wa Uchaguzi Kailima Ramadhani.
Katika Mazungumzo hayo,
Dk. Shein aliupongeza uongozi huo kwa kuendeleza umoja na mashirikiano uliopo
kati ya (NEC) na (ZEC) na kusisitiza haja ya kuendelezwa ili kuendelea
kuijengea sifa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuendelea kufanya kazi zao
kwa ufanisi mkubwa.
Alieleza kuwa
mashirikiano ya pamoja yatasaidia kwa kiasi kikubwa kuendeleza majukumu kwa
Tume zote mbili hasa ikizingatiwa kuwa kila upande una uzoefu wake ambapo kwa
Zanzibar masuala ya uchaguzi hasa wa vyama vingi yalianza tokea mwaka 1957 na
baadae kuendelea hadi hivi leo.
Dk. Shein alitumia
fursa hiyo kueleza matumaini yake makubwa aliyonayo kutokana na uongozi huo wa
NEC, chini ya Mwenyekiti wake Jaji Kaijage kutokana na kuanza vyema majukumu
waliyopewa.
Alieleza kuvutiwa na
mafanikio yaliopatikana na Tume hiyo kutokana na kutekeleza majukumu yao vyema yakiwemo
ya kuhakikisha wananchi wanatumia haki yao ya msingi ya kupiga kura, wanaendesha
chaguzi, wanasimamia na hatimae wanatoa matokeo kwa wakati.
Rais Dk. Shein alieleza
kuwa ana matumaini makubwa kuwa Mwenyekiti huyo ataendeleza vyema majukumu yake
kama alivyofanya Mwenyekiti aliyekuwa kabla yake Jaji Mstaafu Damiani Lubuva
ambaye muda wake wa kushika wadhifa huo umemaliza kwa kutoa mashirikiano mazuri
na NEC sambamba na kutekeleza vyema majukumu yake.
Pamoja na hayo, Rais
Dk. Shein alieleza kuwa suala la Tume hiyo kuwa na Ofisi zake za kudumu hapa
Zanzibar ni suala la lazima na juhudi za makusudi zitachukuliwa na Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar katika kuhakikisha hilo linafanikiwa ili kuweza
kurahishisha shughuli za Tume hiyo hapa Zanzibar na kuweza kuimarisha
mashirikiano na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) hatua ambayo pia, itaweka
ukaribu kati ya NEC na wadau wake hapa Zanzibar.
Aidha, Dk. Shein
aliuhakikishia uongozi huo kuwa ataendelea kutoa ushirikiano wake kwa kutambua
kazi na majukumu makubwa ya Tume hiyo hapa nchini.
Nae Jaji Semistocles Kaijage
alitoa pongezi zake kwa Rais Dk. Shein kwa kuendelea kuingoza vyema Zanzibar
kutokana na ushindi mkubwa alioupata katika Uchaguzi Mkuu uliopita ambao umemuwezesha
kuendelea kuiongoza Zanzibar kwa kipindi cha pili.
Aidha, Jaji Kaijage
alitoa pongezi kwa Rais Dk. Shein kutokana na mashirikiano mazuri inayopata
Tume hiyo kutoka kwa viongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar sambamba na
kuimarika kwa mashirikiano kati ya Tume hiyo na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar
(ZEC).
Jaji Kaijage alimueleza
Dk. Shein majukumu ya Tume hiyo pamoja na juhudi za makusudi zinazochukuliwa na
Tume hiyo katika kuhakikisha inatekeleza vyema majukumu yake ikiwa ni pamoja na
kuendesha Uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wabunge na
Madiwani kwa upande wa Tanzania Bara.
Aliongeza kuwa ili
jukumu hilo lifanyike kwa ufanisi wananchi waliotimiza vigezo vya kupiga kura
na wale wanaotarajia kupiga kura miaka ijayo lazima wapate elimu sahihi ya
Mpiga Kura jambo ambalo wamekuwa wakilitekeleza kwa nguvu zao zote katika
kuhakikisha elimu hiyo inatolewa na Tume hiyo.
Aliongeza kuwa katika
kupanua wigo wa utoaji wa elimu ya Mpiga Kura kwa wananchi wengi zaidi (NEC)
imekuwa ikishiriki katika mikutano mbali mbali ya viongozi ili kutoa elimu
hiyo, wameshakutana na wadau wao wakiwemo viongozi wa vyama vya siasa Tanzania
Bara na Zanzibar, kutoa elimu kupitia vyombo vya habari, uimarishaji wa Daftari
la Kudumu la Wapiga Kura pamoja na kutoa elimu ya Mpiga Kura kwa skuli za
Sekondari katika baadhi ya Mikoa ya Tanzania Bara.
Sambamba na hayo, Jaji
Kaijage alimueleza Rais Dk. Shein kuwa tayari Tume anayoiongoza imeshasimamia
chaguzi sita za Ubunge ukiwemo uchaguzi wa Jimbo la Dimani hapa Zanzibar na chaguzi nyengine tano za Ubunge na Chaguzi
79 za Madiwani huko Tanzania Bara.
Mwenyekiti huyo wa Tume
ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) alimueleza Rais Dk. Shein juhudi zinazoendelea
kufanyika za kujenga jengo jipya la Ofisi za Tume hiyo huko Dodoma na
kusisitiza haja ya kuwa na Ofisi zao za kudumu hapa Zanzibar na kufurahishwa na
azma ya Rais Dk. Shein ya kuhakikisha hilo linafanikiwa katika kipindi kifupi
kijacho kama ilivyo kwa Ofisi nyengine za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania ambazo tayari zina Ofisi zao hapa Zanzibar.
Rajab Mkasaba,
Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment