Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mohammed Aboud Mohammed kulia akizungumza na Ujumbe wa Mwezi Mwekundu wa Emarates kuhusiana na utiliaji saini Ujenzi wa Nyumba za msaada kwa waathirika wa mafuriko Zanzibar.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mohammed Aboud Mohammed aliesimama kulia akiwa pamoja na Msaidizi Balozi wa Emarates Muhammed Ibrahim Al-Bahri wakishuhudia utiaji saini Ujenzi wa Nyumba za msaada kwa waathirika wa mafuriko Zanzibar.
Mkurugenzi wa Kamisheni ya Maafa zanzibar Shaaban Seif Mohammed akibadilishana hati ya saini na Mkurugenzi wa Maafa wa Emarates Said Mohammed Al-humaini kuhusiana na Ujenzi wa Nyumba za msaada kwa waathirika wa mafuriko Zanzibar.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mohammed Aboud Mohammed akiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe wa Mwezi Mwekundu wa Emarates baada ya kutiliana saini Ujenzi wa Nyumba za msaada kwa waathirika wa mafuriko Zanzibar.
Picha na Yussuf Simai - Maelezo Zanzibar.
Na Miza Kona-Maelezo Zanzibar.
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imetiliana saini ya makubaliano na Se rikali ya Nchi za Falme za Kiarabu (UAE), kuhusiana na ujenzi wa nyumba kwa aj ili ya wananchi ambao makaazi yao ya liharibika kutokana na mvua za masi ka.
Hafla hiyo ya utilianaji wa saini hiyo umefanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Vuga Zanzibar. kati ya Mamlaka ya Mwezi Mwekundu ya UAE itakayoshughulikia ujenzi huo na K amisheni ya Maafa ya Zanzibar.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mohammed Aboud Mohammed, amesema msaada wa ujenzi huo ni matu nda ya ziara iliyofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein katika Nchi za Umoja wa Nchi za Falme za Kiarabu mwezi ulipita.
Katika ziara hiyo, Mfalme wa UAE aliahidi kuisaidia Zanzibar katika sekta mbalimbali za maendel eo na huduma za kijamii.
“Tunaishukuru serikali ya UAE kwa msaada huu mkubwa ambao utazidi kuimarisha uhusiano na udugu uliop o baina ya nchi zetu,” alisema Aboud.
Nae Mkurugunzi wa kamisheni ya kuka biliana na Maafa Shaaban Seif Mohammed, amesema msaada huo utasaidia kuond oa usumbufu wanaopata wananchi kat ika kipindi cha mvua hasa yanapotokea mafuriko.
“ Wananchi wanaoishi maeneo ya Ziwa M aboga, Mwanakwerekwe na mengine yanayotu wama maji ndio watakaohamishiwa kw enye nyumba hizo ili wakae katika ma kaazi salama,” alisema.
“ Aidha nyumba zilizojengwa katika m aeneo yenye kupita au kukaa maji tutazivunja ili kukomes ha maafa na usumbufu,” alieleza Mkurugenzi huyo.
Mkurugenzi huyo amewataka wananch i kuchukua tahadhari za mapema kwa k uondoka maeneo yanayokaa maji ili k uepuka na hasara na matatizo waka ti wa kipindi cha mvua.
Nae mwakilishi kutoka ubalozi wa UA E Mohammed Ibrahim Al-Bahr, amesema serikali ya nchi yake itaen delea kuisaidia Zanzibar kwa kuimarisha huduma za kijamii ik iwemo hospitali na uchimbaji wa vis ima kwa lengo la kuwasaidia wananchi wake pamoja na kutemaendelea.
Ameishukuru Serikali ya Zanzibar kwa kuwapatia ardhi itakayotumika kujenga nyumba za makaazi ya kudumu kwa ajili ya wananchi waliokumbwa n a maafa ili waishi kwa furaha na utul ivu.
Mradihuoutahusishanyumba 55 ambapo 30 zitajengwaFukuchaniMkoawaKaska ziniUnguja, nanyengine 25 zitajengwaTumbeMkoawaKaskazini Pemba.
MWISHO.
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR.
Mnaleta warabu watakupindueni.
ReplyDeleteBaniani mbaya kiatu chake dawa