Habari za Punde

Wajumbe wa bodi ya wakurugenzi wa shirika la bandari Zanzibar wakagua maeneo ya Shirika kisiwani Pemba


 MAKAMU Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa shirika la bandari Zanzibar, Khamis Silima Ali mwenye kalamu, akionyeshwa ramani ya eneo la bandari katika mnara wa kuongozea Meli za kimataifa ulioko Kigomasha Makangale Wilaya ya Micheweni, wakati wajumbe wa bodi hiyo walipofanya ziara ya kutembelea maeneo yaliyochini ya shirika hilo.(PICHA NO:ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 WAJUMBE wa bodi ya wakurugenzi wa shirika la bandari Zanzibar, wakionyeshwa mipaka ya eneo la mnara wa kuongozea meli za kimataifa ulioko Kigomasha Makangale Wilaya ya Micheweni, kutoka kwa mkuu wa kituo hicho Yahaya Hassan, wakati wajumbe hao walipofanya ziara ya kukagua maeneo yaliyochini ya shirika hilo upande wa Pemba.(PICHA NO:ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 WAJUMBE wa bodi ya wakurugenzi wa shirika la bandari Zanzibar, wakiongozwa na Makamu mwenyekiti wa bodi hiyo Khamis Salim Ali, wakikagua mipaka ya eneo la Mnara wa Kigomasha Makangale, mnara huo ambao hutumika kuongoza meli za kimataifa.(PICHA NO:ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 MKURUGENZI Mkuu wa Shirika la bandari la Zanzibar Abdalla Juma Abdalla, akitoa maelekezo juu ya bandari ya Wete kwa wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya shirika la bandari, wakati wajumbe hao walipofanya ziara ya kutembelea meneo ya shirika hilo.(PICHA NO:ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 INJINIA Mkuu wa shirika la bandari la Zanzibar Mbarouk Hamad Mbarouk, akitoa maelezo ya kitaalamu juu ya bandari yaw ate, kwa wajumbe wa bodi ya wakurugenzi wa shirika la bandari Zanzibar, wakati walipofanya ziara ya kutembelea maeneo mbali mbali yaliyochini ya bandari tawi la Pemba.(PICHA NO:ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 MKURUGENZI wa shirika la Bandari tawi la Pemba Hamad Salim Hamad, akimuelezea jambo Makamu Mwenyekiti wa bodi ya shirika la Bandari Zanzibar, wakati alipotembelea bandari ya wete katika ziara yao ya kukagua maeneo ya shirika hilo Pemba.(PICHA NO:ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 MMOJA ya nyumba za TRA ambazo zimeshachakaa katika bandari ya Wete, ambazo bodi ya wakurugenzi wa shirika la bandari Zanzibar, wameagiza nyumba hizo kurudishwa kwenye shikila la bandari.(PICHA NO:ABDI SULEIMAN, PEMBA)
 WATENDAJI wa Shirika la bandari Tawi la Pemba, wakimuonyesha Makamu Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa shirika la Bandari Zanzibar, mipaka ya eneo la bandari ya Wete wakati wajumbe hao walipofanya ziara ya kukagua eneo la bandari hiyo.(PICHA NO:ABDI SULEIMAN, PEMBA)
WATENDAJI wa Shirika la bandari Tawi la Pemba, wakimuonyesha Makamu Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa shirika la Bandari Zanzibar, mipaka ya eneo la bandari ya Wete wakati wajumbe hao walipofanya ziara ya kukagua eneo la bandari hiyo.(PICHA NO:ABDI SULEIMAN, PEMBA)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.