MHANDISI ujenzi wa barabara kutoka wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji Khamis Massoud, akionesha hatua ya uwekaji wa lami baridi ulipofikia, kwenye ujenzi wa barabara ya Kuyuni-Ngomeni wilaya ya Chake chake, ikiwa ni agizo maalum la Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Mhe: Dk Ali Mohamed Shein, (Picha na Haji Nassor).
ENEO la
barabara ya Kuyuni –Ngomeni yenye urefu wa kilomita 5.5, ambapo tayari kilomita
1.3 zimeshatiwa lami, na kilomita 2.2 zilizobakia, zikitarajiwa kukamilika kabla
ya mwezi Machi kumalizika, ambapo ujenzi wa barabara hiyo ni agizo la rais wa
Zanzibar,
Picha na Haji
Nassor-Pemba.
NA HAJI NASSOR,
PEMBA.
WASTANI wa wananchi 177 wa kijiji cha Ngomeni shehia ya
Mgelema wilaya ya Chakechake Pemba, wanaendelea kutengenezewa barabara yao kwa
kiwango cha lami, ikiwa ni agizo maalumu la rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
baraza la Mapinduzi Mhe: Dk Ali Mohamed Shein.
Wananchi
hao awali, walitoa kilio chao cha ukosefu wa barabara ya kisasa, mbele ya rais
wa Zanzibar wakati alipowatembelea mwaka jana, ndipo alipoitaka wizara husika,
kuhakikisha wanaitengeneza ili iweze kupitika kipindi chote.
Baada
ya wizara kukamilisha hatua hiyo, wananchi hao walimuomba tena rais huyo wa
Zanzibar, sasa kuwajengewa kwa kiwango cha lami, ambapo tayari ujenzi huo
umeshaanza na kabla ya kumalizika kwa mwezi Machi mwaka huu, itakuwa
imeshakamilika.
Ujenzi huo unaofanywa na Wizara ya Ujenzi,
Miundombinu na Usafirishaji Zanzibar, kwa kiwango cha lami, umaenza miezi
mitatu iliopita, na unatarajiwa kukamilika wakati wowote kabla ya mwisho wa
mwezi ujao.
Mhandisi
ujenzi wa wizara hiyo, Khamis Massoud, alisema hatua ya utiaji wa lami baridi
ulishakamika tokea Febuari 16, ndipo hatua ya uwekaji wa lami moto ulipoanza
mapema siku tatu baadae, na wanaendelea kwa kasi.
Alisema
kama mashine yao moja ilioharibika juzi wa mafundi wataiweza, basi hatua ya
kumalizia kilomita 2.2 ziliobakia kwa utiaji wa lami moto, utakamilika sio
chini ya wiki tatu zijazo.
Alisema
kwa sasa tayari kilomita 1.3 zimeshakamilika kwa utiaji wa lami, na sasa
wanajipanga ili kuweka alama za barabarani na baada ya kuimaliza yote kilomita
5.5 wataikabidhi serikalini, kwa hatua za ufunguzi.
“Kwa
sasa kazi ya uwekaji lami baridi tumeshakamilisha, na kazi inayoendelea kwa
kasi kubwa ni umaliziaji wa uwekaji wa lami moto, na naamini kabla kumalizika
mwezi ujao, na sisi tutakuwa tumeshamaliza kazi,”alisema Mhandisi huyo.
Wakati
huo huo Mhandisi huyo, alisema wakikamilisha kazi hiyo, watakwenda kwenye
barabara ya Kangani- Mkanyageni yenye urefu wa kilomita 5, kwa kufanya
matengenezo ya madogo ya kifusi, na kisha uwekaji wa lami.
Sheha
wa shehia ya Mgelema Omar Idd Zaina, alisema kwa sasa wananchi wake pamoja na yeye
mwenyewe, wamefurahishwa kuona rais analoliahidi analitekeleza kwa wakati.
“Sisi
kwa kijiji cha Ngomeni tuko sawa kama wa mjini Chakechake, maana maji yapo,
umeme safi, barabara tayari na hospitali keshokutwa,”alisema sheha huyo.
Nae
mwananchi Asha Muhsin, alisema sasa hawatakuwa tena na shida, wanapotaka kwenda
mjini kwa ajili ya shughuli zao mbali mbali.
“Ilikuwa
ukitaka kwenda mjini hasa siku za mvua, kwanza ujipange vyema maana kwanza
hakuna hata gari ya abiria, lakini sasa karibu tutapata hata usafiri wa
umma,”alisema.
Mshauri
wa rais Pemba Mauwa Abeid Daftari, alisema usafiri wa barabarani
duniani kote,
ndio kifaa pekee cha kuwafikishia maendeleo wananchi.
“Mimi
kwanza nimshukuru sana rais wetu, kwa kuamua kutekeleza ahadi zake kwa wananchi
hawa, na huku ndio kutelekeza Ilani ya CCM kwa vitendo,”alisema.
Barabara
hiyo yenye urefu wa kilomita 5.5, kwenye miaka ya 75 ilikuwa ikitumiwa na
waenda kwa miguu, kabla ya kuanza kuwa kwa ajili ya gari za Ng’ombe na Punda
ambapo 14 baadae , ilianzishwa na wakulima wa karafuu na sasa mwaka 2018 in ya
kiwango cha lami.
No comments:
Post a Comment