Kaimu
Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA),
Bw. Johannes Munanka akijibu maswali ya wafanyakazi wa kiwanja hicho, leo
alipokutana nao katika mkutano uiliofanyika katika ukumbi wa Transit ulipo
Jengo la Kwanza la abiria (TBI).
Wafanyakazi
wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa
cha Julius Nyerere (JNIA), wakimsikiliza kwa makini Kaimu Mkurugenzi wa
kiwanja hicho, Bw. Johannes Munanka
leo alipokuwa akizungumza nao mambo mbalimbali ya kazi.
Afisa
Uendeshaji wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA),
Bi. Rachel Manyilizu akiuliza maswali kwa Kaimu Mkurugenzi wa JNIA (hayupo
pichani) katika mkutano wa wafanyakazi uliofanyika kwenye ukumbi wa
Transit katika jengo la Kwanza la abiria (TBI).
Fundi
Umeme Mwandamizi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere
(JNIA), Bi Mastidia Ndyomulwango akiwasilisha hoja kwenye mkutano wa
Wafanyakazi wa JNIA, ulioitishwa na Kaimu Mkurugenzi wake, Bw. Johannes
kujadili masuala mbalimbali ya kiutendaji wa kazi.
Afisa
Usalama, Bw. Musso John, akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali
yaliyoulizwa katika mkutano ulioitishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Kiwanja cha
Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Johannes Munanka
uliofanyika leo kwenye ukumbi wa Transit uliopo katika Jengo la Kwanza la
abiria (TBI).
Meneja Uendeshaji wa Kiwanja cha Ndege cha
Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw.
Vedastus Fabian (mwenye miwani mbele) akiandika mambo mbalimbali katika mkutano
ulioitishwa na Kaimu Mkurugenzi wa JNIA, Bw. Johannes Munanka ambaye hayupo
pichani.
Na
Mwandishi Wetu
KAIMU
Mkurugenzi wa Kiwanja CHA Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw.
Johannes Munanka amewataka wafanyakazi kufanya kazi kwa bidii na juhudi ili
kuongeza tija na kukuza uchumi wa nchi.
Bw.
Munanka alitoa kauli hiyo leo alipokutana na wafanyakazi wa JNIA, katika mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa
mikutano wa Transit uliopo Jengo la Kwanza la abiria (TBI), ambapo amesema
wafanyakazi wasipofanya kazi kwa bidii watashindwa kuzalisha kwa ziada. Huduma
kubwa inayotoa JNIA ni pamoja na kutua na kuruka kwa ndege za ndani na nje ya
nchi.
Amesema
wafanyakazi wasiofanyakazi kwa bidii watasababisha kuzorota kwa utoaji wa
huduma kwenye Kiwanja hiki, jambo ambalo litasababisha kukimbiza abiria na
wateja wengine wanaofanya shughuli zao mbalimbali kwenye kiwanja hiki, ambacho
ni miongoni mwa viwanja viwili vya Kimataifa vilivyopo nchini. Kiwanja kingine
cha Kimataifa ni cha Kilimanjaro (KIA).
“Ninawashukuru
sana wafanyakazi wanaochapa kazi kwa bidii bila kusukumwa ingawa wengine asili
ya kazi zao zinawasukuma kufanya hivyo, mfano mzuri ni waongoza ndege hawezi
kutegea, tofauti na wachache waliopo katika idara nyingine wamekuwa hawana
bidii ya kazi hadi wasukumwe,” amesema Bw. Munanka.
Hata
hivyo, amesema wafanyakazi wote wanaosubiri kusukumwa waache mara moja na
wahakikishe wanajituma wenyewe, ili kuboresha huduma zinazopatikana JNIA,
ambazo zitakuwa sifa nzuri ya kuvuta wateja kutoka ndani na nje ya nchi.
“Ukiangalia
katika ngazi ya meneja au wanaoingia kwenye menejimenti nao wanatakiwa
kuwasimamia kwa umakini mkubwa na endapo watashindwa kufanya hivyo inanilazimu
nifanye kazi za kusimamia na umeneja, ambapo sio jambo zuri litasababisha
kushindwa kutekeleza majukumu mengine zaidi ya kiutendaji, hivyo ndugu zangu
tuchape kazi,” amesema Bw. Munanka.
Akizungumzia vitendea kazi, Bw. Munanka ameahidi kushughulikia kwa ngazi ya JNIA ili vipatikane haraka na pia kuwasilisha Makao Makuu (Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania-TAA) vile vinavyohitaji idhini ya kuvinunua
No comments:
Post a Comment