Naibu Waziri wa
Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (kushoto) akizungumza na
waandishi wa habari baada ya kufanya mazungumzo na msanii wa muziki Ney Wamitengo kuhusu namna ya
kuboresha na kufuata maadili ya mtanzania katika kazi ya sanaa anayoifanya leo
Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Bw.
Godfrey Mngereza
Afisa Utangazaji
kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Bw. Rolf Kibaja akizungumza
wakati wa kikao cha Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo
Mhe. Juliana Shonza kuzungumza na waandishi wa habari baada ya kufanya
mazungumzo na msanii wa muziki Ney Wamitengo kuhusu namna ya kuboresha na
kufuata maadili ya mtanzania katika kazi ya sanaa anayoifanya leo Jijini Dar es
Salaam.
Katibu Baraza la
Sanaa la Taifa (BASATA) Bw. Godfrey Mngereza (kulia) akifafanua jambo wakati wa
kikao cha Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana
Shonza (kushoto) kuzungumza na waandishi wa habari baada ya kufanya mazungumzo
na msanii wa muziki Ney Wamitengo kuhusu namna ya kuboresha na kufuata maadili
ya mtanzania katika kazi ya sanaa anayoifanya leo Jijini Dar es Salaam.
Msanii wa kizazi
kipya Emmanuel Elibariki (Ney Wamitego) (kulia) akizungumza na waandishi wa
habari wakati wa kikao cha Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na
Michezo Mhe. Juliana Shonza (kushoto) kuzungumza na waandishi wa habari baada
ya kufanya mazungumzo naye kuhusu namna ya kuboresha na kufuata maadili ya
mtanzania katika kazi ya sanaa anayoifanya leo Jijini Dar es Salaam.
Picha
na:
Genofeva Matemu -WHUSM.
Na: Genofeva Matemu –
WHUSM.
Naibu Waziri wa
Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza amemfungia msanii wa
muziki wa kizazi kipya Ibrahim Musa (Roma Mkatoliki)
kutofanya kazi yoyote ya sanaa ikiwemo kutokufanya maonyesho ya sanaa ya
majukwaa kwa kipindi cha miezi sita na kumtaka Msanii Emmanueli Elibariki (Ney
Wamitego) kuacha kutumia maneno yenye utata yanayolenga kuleta mmomonyoko wa maadili
ya mtanzania anapoandaa nyimbo zake.
Mhe. Shonza ametoa
agizo hilo leo jijini Dar es Salaam baada ya msanii Roma Mkatoliki kuitwa na
BASATA mwaka jana na kukubaliana kurekebisha kasoro zilizojitokeza katika wimbo
wake wa kibamia lakini hadi sasa msanii huyo kukiuka makubaliano hayo na
kukiuka agizo la Naibu Waziri la kumtaka
kufika ofisini kwake leo kwa ajili ya kufanya mazungumzo yanayolenga kuwekana
sawa katika uandaaji wa kazi za sanaa.
“Kwa upande wa msanii
Roma Mkatoriki aliyeimba wimbo wa kibamia ambaye ameshaitwa na BASATA kufanyia
marekebisho ya wimbo huo na kukubali kufanyia marekebisho kasoro zilizopo
lakini hadi sasa hakuna marekebisho yoyote yaliyofanyika na kibaya zaidi wimbo
huo unaendelea kupingwa kwenye vyombo vya habari; natangaza kuwa namfungia msanii Roma Mkatoliki kwa kipindi cha miezi sita haruhusiwi kufanya
kazi yoyote ya sanaa lakini pia hakuna kufanya maonyesho yoyote ya sanaa kwenye
majukwaa kwa kipindi hicho cha miezi sita” amesema Mhe. Shonza
Aidha Mhe. Shonza
amesema kuwa japo serikali inatambua kuwa sanaa ni ajira, lakini ajira hii
imekua ikitumika vibaya kwa kuharibu maadili ya mtanzania kulingana na maneno
yanayotumika sambamba na kuwa na mavazi ya uchi katika picha jongevu hivyo
kudhalilisha utu hasa kwa mwanawake.
“Msanii Ney wa Mitego
tumemuonya kutokana na nyimbo anazozitoa kutumia maneno yenye utata na wakati
mwingine kuwa na picha jongevu zinazodhalilisha utu wa mtu na kukubaliana nasi
kuwa atabadilika na kuzingatia maadili ya mtanzania kwa kazi zake za mbeleni”
amesema Mhe. Shonza
Hali kadharika Mhe.
Shonza ameitaka BASATA kuanzia sasa inapotokea kuwa wimbo unatolewa na msanii
yeyote na unakiua maadili ya mtanzania wimbo huo uchukuliwe hatua kwa haraka
bila kupoteza muda katika kuhakikisha kwamba sanaa kama msingi muhimu wa
kuburudisha na kuelimisha inazingatia miiko na maadili yaliyowekwa na vyombo
vinavyosimamia sekta ya sanaa
Kwa upande wake Afisa
Utangazani kutoka Mamlaka ya Mawasiliano ya Tanzania (TCRA) Bw. Rolf Kibaja
ametoa rai kwa vituo vyote vya utangazaji nchini kuzingatia kanuni za
utangazaji kwasababu vituo hivyo vinapopewa leseni hupewa na sheria na kanuni
za uendeshaji wa vituo hivyo; hivo kuwataka waandaaji na wasimamizi wa vipindi
kuzingatia kanuni hizo kwani Mamlaka ya mawasiliano imejipanga kuhakikisha kuwa
nyimbo zote zitakazokua zinaenda kinyume na maadili zitachukulia hatua kwa
mujibu wa sheria kanunu na taratibu zilizopo.
Naye Katibu Mtendaji
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Bw. Godfrey Mngereza amesema kuwa Baraza
halina budi kutumia kanuni na sheria zilizopo kuwajibisha kazi za sanaa ambazo
zinaathiri jamii ya kitanzania kimaadili na kuwataka wasanii kufuata misingi imara ya kuelimisha na kuburudisha
kuliko kuleta athari katika jamii hasa kwa kizazi cha leo na cha kesho.
Sanjari Msanii Ney
Wamitego ameishukuru wizara inayosimamia sekta ya sanaa kwa kumweka sawa na
kumpa nafasi nyingine yakuweza kujirekebisha katika kazi zake za sanaa na
kuahidi kufanya mazuri mengi ambayo yatakuwa tofauti na aliyowahi kufanya
awali.
No comments:
Post a Comment