Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akimuapisha Waziri wa Biashara na Viwanda Balozi Amani Salum Ali, Hafla hiyo imefanyika leo Ikulu Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed
Shein leo amewaapisha viongozi
aliowateua hapo jana kushika nyadhifa mbali mbali katika Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar.
Hafla hiyo,
ilifanyika Ikulu mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa
Serikali ambapo viongozi walioapishwa
ni Waziri wa Biashara na Viwanda Balozi Amina Salim Ali, Waziri wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo Balozi Ali Abeid
Karume, Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji Dk. Sira Ubwa Mamboya.
Wengine ni
Waziri wa Afya, Hamad Rashid
Mohamed, Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Rashid Ali Juma, Waziri wa Ardhi, Nyumba, Maji na
Nishati Salama Aboud Talib, Waziri
wa Habari, Utalii na Mambo ya Kale
Mahmoud Thabit Kombo, Waziri
wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto
Maudline Cyrus Castico,
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba, Maji na
Nishati, Juma Makungu Juma, Naibu Waziri wa Habari, Utalii na Mambo ya Kale
Choum Kombo Khamis, Naibu Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto
Shadia Mohamed Suleiman, Naibu
Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Dk. Makame Ali Ussi, Naibu Waziri wa Biashara na Viwanda
Hassan Khamis Hafidh.
Pia,
Dk. Shein aliwaapisha Wakuu wa Wilaya aliowateua hapo jana ambao ni Issa Juma Ali alieapishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mkoani, Pemba na Rajab Ali Rajab alieapishwa kuwa Mkuu wa
Wilaya ya Kaskazini B, Unguja.
Viongozi mbali mbali walihudhuria katika
hafla hiyo akiwemo Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd, Spika wa Baraza
la Wawakilishi Zubeir Ali Maulid, Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu, Mwanasheria Mkuu wa
Zanzibar Said Hassan Said, Mawaziri, Manaibu Mawaziri na Wakuu wa Mikoa.
Wengine waliohudhuria ni Mufti Mkuu wa
Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabih,Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji,
Wakuu wa Vikosi vya SMZ, Washauri wa Rais wa Zanzibar pamoja na viongozi
wengine wa Serikali.
Nao viongozi hao walioapishwa waliahidi kuendelea
kumsaidia Rais Dk. Shein katika kuhakikisha Zanzibar inazidi kupata maendeleo,
waliahidi kuimarisha mashirikiano ya dhati katika kuwatumikia wananchi, kuleta
mabadiliko na kufanya kazi kwa vitendo sambamba na kuendelea kusimamia amani na
utulivu uliopo nchini.
Hapo
jana, Dk. Shein alifanya mabadiliko madogo katika Baraza la Mapinduzi kwa
kuongeza Wizara moja zaidi na kuwabadilisha Wizara baadhi ya Mawaziri.
Kufuatia
mabadiliko hayo, shughuli za Vijana zimehamishiwa katika Wizara mpya ya Vijana,
Utamaduni, Sanaa na Michezo shughuli za Mazingira zimehamishiwa katika Ofisi ya
Makamu wa Pili wa Rais na shughuli za Wakala wa Serikali wa Uchapaji
zimehamishiwa Wizara mpya ya Habari, Utalii na Mambo ya Kale.
Aidha,
amewateua Naibu Mawaziri wapya wawili na kumbadilisha Wizara Naibu Waziri mmoja
ambapo kufuatia mabadiliko hayo, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar hivi sasa
itakuwa na Wizara 14.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment