|
TUME
YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA
Kitalu
Na. 8, Mtaa wa Luthuli
S.L.P
2643, DAR ES SALAAM
Simu:
+255 22 2135747/8; 2137125; 2135222
Faksi:
+255 22 2111281
Tovuti:
www.chragg.go.tz
|
Juni 13,2018
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
SIKU YA KIMATAIFA YA KUHAMASISHA UELEWA KUHUSU
MASUALA YA UALBINO
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora inaungana na wadau wote wanaolinda na kutetea haki za watu wenye ualbino nchini kwenye kuadhimisha siku ya Kimataifa ya kutoa Elimu kuhusu dhana na haki za watu wenye ualbino duniani “International Albinism Awareness Day’’ tarehe 13/06/2018 ikiwa na kauli mbiu “KUANGAZA MWANGA WETU ULIMWENGUNI”. Kitaifa maadhimisho haya yatafanyika Mkoani Simiyu.
Siku hii
imepitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa Azimio Na. A/HRC/RES/23/13
la terehe 18/12/2014. Tanzania ni mwanachama hai wa Baraza hilo, hivyo kama
nchi tunapaswa kuishi tamko la Umoja wa Mataifa kwa vitendo na kutekeleza
yaliyokubaliwa.
Tume kwa kushirikiana na wadau
mbalimbali nchini tunaendelea kutetea haki za watu wenye ualbino na kuweka
msukumo wa utekelezaji wa Sheria ya Watu wenye Ulemavu ya mwaka 2010.
Watanzania wanatakiwa kuachana na
imani potofu za kishirikina za kuwaua, kuwanyanyapaa, kuwabagua na kuwatesa
watanzania wenzetu wenye ualbino. Matukio ya ukatili, unyanyasaji, na mauaji
kwa watu wenye ualbino yamepungua kwa kiasi nchini. Katika hili Tume inapenda
kipekee kutambua juhudi kubwa za Serikali na wadau wote katika kuhakikisha ulinzi
na usalama wa watu wenye ualbino. Wenzetu wenye ualbino wanakabiliwa na
changamoto zingine za kielimu, kiafya na kijamii na unyanyapaa ambapo juhudi zaidi
kutoka kwa wadau wote zinahitajika.
Aidha, Tume inaiomba Serikali kuendeleza
juhudi zake za kuhakikisha upatikanaji wa vifaa tiba (sunscreen lotions) na
vifaa saidizi vya kielimu kwa watu wenye ualbino ili waweze kushiriki
kikamilifu katika kutoa mchango wao katika kujenga Taifa letu.
Tume inaahidi kuendelea
kushirikiana na wadau wote katika kuhakikisha haki za watu wenye ulemavu
wakiwemo watu wenye ualbino zinalindwa, zinakuzwa na kutetewa nchini.
Imetolewa na:
SIGNED
Mary Massay
KATIBU
MTENDAJI
No comments:
Post a Comment