Habari za Punde

Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi ya Taifa NEC Atembelea Ujenzi wa Ofisi za NEC Dodoma.

 Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Dkt. Athumani Kihamia (kushoto) akizungumza na baadhi ya Watendaji wa Wakala wa Majengo nchini (TBA) na wataalam kutoka Chuo Kikuu Ardhi mara baada ya kutembelea eneo la mradi wa Ujenzi wa Ofisi za NEC, Njedengwa jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi ya  Dkt. Athumani Kihamia (kulia) akizungumza jambo na Mhandisi wa Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutoka TBA alipofanya ziara ya kutembelea eneo la ujenzi wa ofisi hizo Njedengwa , jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi ya Taifa,Dkt. Athumani Kihamia (katikati) akikagua eneo linapojengwa ghala la kuhifadhia vifaa vya Uchaguzi akiwa ameambatana na baadhi ya Maafisa wa NEC na  wataalam  wanaojenga  mradi huo  kutoka TBA.
Jengo la Utawala la Tume ya Taifa ya Uchaguzi likiwa katika hatua za ujenzi katika eneo la Njedengwa jijini Dodoma.
Mhandisi wa Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za NEC jijini Dodoma Mhandisi Yohana Mashauri (kulia) akimweleza jambo Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Dkt. Athumani Kihamia aliyetembelea ujenzi wa Ofisi hizo.
Baadhi ya watendaji na Wasimamizi wa Mradi wa ujenzi wa Ofisi za NEC jijini Dodoma wakimsikiliza Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Dkt. Athumani Kihamia (hayupo pichani).

Mhandisi wa Mradi wa Ujenzi wa Ofisi za NEC jijini Dodoma Mhandisi Yohana Mashauri (kushoto) akitoa ufafanuzi kwa Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Dkt. Athumani Kihamia (wa pili kutoka kushoto) wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Ofisi hizo jijini Dodoma.
 Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Dkt. Athumani Kihamia (katikati) akikagua eneo linapojengwa ghala la kuhifadhia vifaa vya Uchaguzi akiwa ameambatana na baadhi ya Maafisa wa NEC na  wataalam  wanaojenga  mradi huo  kutoka TBA.
Picha na NEC – Dodoma

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.