Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Mhe. Lt. Mstaafu Chiku Galawa mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa kimataifa wa ndege wa Songwe tayari kwa ziara ya siku 5
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimia na Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa kimataifa wa ndege wa Songwe tayari kwa ziara ya siku 5.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongozana na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Mhe. Lt. Mstaafu Chiku Galawa mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa kimataifa wa ndege wa Songwe tayari kwa ziara ya siku 5. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa kimataifa wa ndege wa Songwe tayari kwa ziara ya siku 5.
(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewasili mkoani
Songwe tayari kwa ziara ya siku 5.
Makamu wa Rais
amepokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Mhe. Lt. Mstaafu Chiku Galawa, Mkuu wa
Mkoa wa Mbeya Mhe. Amos Makala pamoja na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni
Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii
Mhe. Japhet Hasunga na Viongozi wengine wa Chama na Serikali.
Akiwa
mkoani Songwe, Makamu wa Rais atakagua na kuhamasisha shughuli mbalimbali za
maendeleo ambapo atatembelea Wilaya Tatu za Mkoa huo ambazo ni Mbozi, Momba na
Ileje. Makamu wa Rais ataanzia ziara yake katika Wilaya ya Mbozi ambapo
miongoni mwa shughuli atakazofanya ni pamoja na kukagua na kufungua kituo cha
Afya Nanyala, kusalimia wananchi katika eneo la mradi la Nanyala, kuweka jiwe
la Msingi katika Mradi wa maji Iyula na kufanya Mkutano wa hadhara katika kijiji
cha Iyula.
Makamu
wa Rais pia atatembelea Wilaya ya Momba ambapo atakagua na kuzindua kituo cha
Afya Tunduma, atakagua shughuli za vikundi vya wajasiriamali Tunduma na kufanya
mkutano wa hadhara kuzungumza na wananchi wa Wilaya ya Momba.
Vilevile,
Makamu wa Rais atatembelea Wilaya ya Ileje ambapo atapokea taarifa ya shughuli
za uhifadhi wa mazingira na upandaji miti na kukagua shughuli za uhifadhi
na shamba la miti la Wakala wa Misitu
Tanzania lilopo Katengele na baadae kufanya mkutano wa hadhara katika kijiji cha Isoko ambapo atapata fursa
ya kuzungumza na wananchi wa Ileje.
Imetolewa na;
Ofisi ya Makamu wa
Rais
Julai 21, 2018
No comments:
Post a Comment