SERIKALI
YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR
WAKALA WA USAJILI WA BIASHARA NA MALI
ZANZIABAR - BPRA
TANGAZO
Wakala wa Usajili wa Biashara
na Mali Zanzibar (BPRA) inapenda kuwajuuilisha wafanyabiashara na wananchi kuwa
imeanza rasmi kutumia mfumo wa usajili kwa kutumia mtandao ‘Online Registration System’
(ORS) kuanzia tarehe 01/07/2018. Huduma zote zinazohusiana na usajili wa
Kampuni, Majina ya Biashara, Jumuiya za Kiraia (NGOs), Vyama vya Ushirika na Mashirika
ya Serikali. Pia usajili wa Amana za Mali Zinazohamishika zinatolewa kupitia mifumo
hiyo kwa anuani ifuatayo:-orsz.bpra.go.tz
Aidha taasisi zote zilizosajiliwa
kabla ya matumizi ya mifumo ya usajili zinapaswa kuingiza taarifa zao kwenye mfumo
wa usajili bila ya malipo kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia tarehe ya kutumika
mfumo huo.
Ili kuweza kutumia mfumo huo muombaji
anapaswa awe na:-
1
.
Kitambulisho cha Mzanzibari Ukaazi ‘Zan
ID’ au Kitambulisho cha Taifa ‘National Identity Card’ kwa raia wa Tanzania.
2. Kwa wageni awe na pasi
ya kusafiria ‘Passport’
3. Anuani ya barua pepe
(email account).
Ada zote zinazohusiana na huduma hizi zitalipwa katika Benki yaWatu wa
Zanzibar ‘The People’s Bank of Zanzibar’
(PBZ) ambapo taarifa zake zinapatikana kwenye mfumo huu.
Kwa maelezo zaidi tembelea tovuti ya BPRA; www.bpra.go.tz,au www.orsz.bpra.go.tz
Imetolewa na Wakala wa Usajili wa Biashara na
Mali Zanzibar (BPRA)
S.L.P 260, Zanzibar – Tanzania
Barua pepe: info@bpra.go.tz
No comments:
Post a Comment