Naibu Waziri wa Mifugo na
Uvivu, Mh. Abdallah Hamis Ulega, akiwa ameongozana na Mwakilishi wa Jumuiya ya
Ulaya (EU), Jenny Correia Nunes, na Mkurugenzi Mkazi wa WWF Tanzania, Dkt.
Amani Ngusani kuelekea baharini kupokea
msaada wa boti mbili za doria zenye thamani ya Shilingi Millioni 144 zilizotolewa na EU kupitia
miradi ya WWF nchini.
Naibu Waziri wa Mifugo na
Uvivu, Mh. Abdallah Hamis Ulega, akiwa ameongozana na Mwakilishi wa Jumuiya ya
Ulaya (EU), Jenny Correia Nunes, na Mkurugenzi Mkazi wa WWF Tanzania, Dkt.
Amani Ngusani kuelekea baharini kupokea
msaada wa boti mbili za doria zenye thamani ya Shilingi Millioni 144 zilizotolewa na EU kupitia
miradi ya WWF nchini.
Naibu Waziri wa Mifugo na
Uvivu, Mh. Abdallah Hamis Ulega, akizungumza na Mwakilishi wa Jumuiya ya Ulaya
(EU), Jenny Correia Nunes, na Mkurugenzi Mkazi wa WWF Tanzania, Dkt. Amani
Ngusani baada ya kuwasili katika Uwanja wa Maalim Kilwa Kivinje mkoani Lindi
Tarehe 26.7.2018 kupokea msaada wa boti mbili za doria zenye thamani ya
Shilingi Millioni 144 zilizotolewa na EU
kupitia miradi ya WWF nchini kwa Wilaya mbili ya Kilwa Kivinje na Mafia
Naibu Waziri wa Mifugo na
Uvivu, Mh. Abdallah Hamis Ulega, Mwakilishi wa Jumuiya ya Ulaya (EU), Jenny Correia
Nunes, na Mkurugenzi Mkazi wa WWF Tanzania, Dkt. Amani Ngusani wakisaini
makubaliano baada ya kupokea msaada wa boti mbili za doria zenye thamani ya
Shilingi Millioni 144 zilizotolewa na EU
kupitia miradi ya WWF nchini kwa Wilaya mbili ya Kilwa Kivinje na Mafia katika Viwanja
wa Maalim Kilwa Kivinje mkoani Lindi Tarehe 26.7.2018
Naibu
Waziri wa Mifugo na Uvivu, Mh. Abdallah Hamis Ulega, akizungumza akipokea mkataba
kutoka Mwakilishi wa Jumuiya ya Ulaya (EU), Jenny Correia Nunes, baada ya kusaini makubaliano ya kupokea msaada wa boti
mbili za doria zenye thamani ya Shilingi
Millioni 144 zilizotolewa na EU kupitia miradi ya WWF nchini kwa Wilaya
mbili ya Kilwa Kivinje na Mafia katika Viwanja wa Maalim Kilwa Kivinje mkoani
Lindi
Naibu
Waziri wa Mifugo na Uvivu, Mh. Abdallah Hamis Ulega, akizungumza akipokea mkataba
kutoka Mwakilishi wa Jumuiya ya Ulaya (EU), Jenny Correia Nunes, baada ya kusaini makubaliano ya kupokea msaada wa boti
mbili za doria zenye thamani ya Shilingi
Millioni 144 zilizotolewa na EU kupitia miradi ya WWF nchini kwa Wilaya
mbili ya Kilwa Kivinje na Mafia katika Viwanja wa Maalim Kilwa Kivinje mkoani
Lindi
Naibu
Waziri wa Mifugo na Uvivu, Mh. Abdallah Hamis Ulega, akizungumza akimkabidhi
mkataba Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Kivinje, ambaye ni RAS baada ya kusaini makubaliano ya kupokea msaada wa boti
mbili za doria zenye thamani ya Shilingi
Millioni 144 zilizotolewa na EU kupitia miradi ya WWF nchini kwa Wilaya
mbili ya Kilwa Kivinje na Mafia katika Viwanja wa Maalim Kilwa Kivinje mkoani
Lindi
Naibu
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe Abdallah Hamis Ulega amekabidhi boti mbili za
doria kwa BMU za Kilwa Kivinje na Mafia. Zoezi hili limefanyika katika
Wilaya ya Kilwa eneo is Kivinje. Boti hizo zina thamani ya fedha za Kitanzania
milioni 144 ambazo zimefadhiliwa na Umoja wa Ulaya kupitia miradi ya WWF.
Mwakilishi
wa Umoja wa Ulaya Bibi Jenny amesema wanafadhili miradi ya WWF hapa Tanzania
yenye jumla ya bilioni 7 za Kitanzania. Aidha, amefurahi kusikia kwa uvuvi wa
mabomu umepungua sana na hii ni sababu ya juhudi za serikali na wananchi wa
maeneo haya. Pia alisema wao wamenunua boti ila jukumu za kuzilinda ni la
Serikali ya Wilaya husika.
Naye Mkurugenzi wa WWF nchini amesema wamepata taarifa kutoka kwa wavuvi kwamba
sasa samaki wanaongezeka na kupatikana kwa samaki ambao walishapotea na haya
yote ni kwa sababu ya kupungua kwa asilimia kubwa uvuvi wa mabomu.
Mhe Ulega Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi amesema Umoja wa Ulaya umenunua
hizi boti kuunga mkono kati kubwa inayofanywa na Mhe Rais John Pombe Magufuli
ya Serikali yake ya awamu ya tano. Alisema amezunguka wilaya za Mkinga, Tanga
Mjini, Muheza, Pangani na Lindi kote huko wavuvi wanakiri samaki wameongezeka
kwa sasa.
Ukanda
huu wa Pwani hauna viwanda vya samaki na kumuomba Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya
kutafuta wawekezaji kuja kuwekeza viwanda vya samaki katika mwambao wa bahari
ya Hindi, pia alimuomba kufadhili ujenzi wa soko la samaki Kilwa Kivinje. Mhe.
Ulega aliwaasa umoja wa vikundi vya BMU kutunza boti hizo na kuwaagiza Wilaya
kusimamia ulinzi wa boti hizo. Mwisho aliwaomba WWF kuwaangalia BMU na wavuvi
wa maeneo mengine kama Mkinga, Pangani, Lindi Vijijini na Mkuranga kwani nao
wana mahitaji ya boti kama hizi katika ulinzi wa rasilimali zetu za bahari.
No comments:
Post a Comment