Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk.Ali Mohamed Shein, akiondoa kipazia kuashiria Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Jengo Jipya la ZURA Maisara leo, ikiwa ni shamrashamra za Kuadhimisha Miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar, kulia Waziri wa Ardhi Nyumba Maji na Nishati Zanzibar Mhe. Salama Aboud Talib.
Jengo la Wizara ya Ardhi Nyumba Maji na Nishati Zanzibar lililopewa jina la ZURA House.likiwa katika ujenzi wake ukiendelea katika eneo la Maisara Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed
Shein amesema kuwa Mapinduzi
ya Januari 12, 1964 yamefanywa kwa lengo la kuleta mabadiliko, uhuru, ukombozi
pamoja na kujenga misingi ya usawa umoja na heshima kwa Wazanzibari wote.
Dk. Shein aliyasema hayo leo mara baada
ya kuweka jiwe la msingi jengo jipya la Ofisi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma
za Maji na Nishati Zanzibar (ZURA) linalojengwa sambamba na Ofisi ya Wizara ya
Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati pamoja na ZURA huko Maisara Mkoa wa Mjini
Magharibi ikiwa ni miongoni mwa shamrashamra za miaka 55 ya Mapinduizi ya Zanzibar.
Rais Dk. Shein
alisema kuwa Mapinduzi matukufu ya Januari 12, 1964 ndiyo yaliyojenga utu wa Wazanzibari na bado yanaendelea kuifanya Zanzibar iweze
kuimarika na kupendwa duniani kote.
“Mapinduzi
yameleta heshima na mabadiliko makubwa ndio maana tunasema Mapinduzi Daima,
kwani leo ni miaka 55 tokea Zanzibar iwe huru”,alisisitiza Dk. Shein.
Alieleza kuwa
katika miaka 55 Zanzibar imefanya mambo makubwa sana ambayo wakoloni
hawakuyafanya lakini mara tu baada ya Mapinduzi, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
imeweza kuyafanya na kuleta mabadiliko makubwa.
Dk. Shein alieleza
umuhimu wa maji kwa mwanaadamu ambayo huduma hiyo inadhibitiwa na mamlaka hiyo na
kusisitiza kuwa bila ya maji mwanaadamu hawezi kuishi na hakuna kiumbe hata
mmoja ambae anaweza kuishi bila ya kuwepo kwa huduma hiyo muhimu.
Hivyo, Rais Dk.
Shein alisisitiza kuwa ni vyema
kukawekwa nidhamu ya matumizi ya maji na ndio maana Serikali zote duniani
zinaanzanisha na kuwezaka Taasisi za udhibiti na ndio maana Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar mnamo mwezi April mwaka, 2015 ikaunda Taasisi hiyo.
“Mwanzo ilipoundwa
Taasisi hii haikufahamika vyema madhumini yake lakini mara baada ya watu kujua
basi kila mmoja alitaka kufanya kazi ZURA na wanasema Kule Mambo yamenoga kwani
mwanzo haikuwa hivyo watu walidharau” alisisistiza Dk. Shein.
Aidha, Rais Dk.
Shein alieleza kuwa kuwepo kwa chombo cha udhibiti katika Serikali ni muhimu sana na hatua hiyo
imeweza kusaidia kwa kiasi kikubwa kuanzisha Taasisi hiyo ambayo pia imeweza
kusaidia kwa kiasi kikubwa katika zoezi la utafutaji wa Mafuta na Gesi hapa
Zanzibar.
Alieleza kuwa
uwekaji wa jiwe la msingi wa jengo hilo kutasaidia kwa kuwaweka wafanyakaazi wa
Wizara hiyo na Taasisi zake pamoja na kupelekea kufanya kazi vyema.
Katika maelezo
yake, Rais Dk. Shein pia, alitumia fursa hiyo kwa kueleza kuwa Maktaba iliopo hivi sasa ambayo iko jirani na jengo hilo la
ZURA itavunjwa NA kujengwa mpya tena ya
kisasa mara baada ya kumaliza jengo hilo jipya kupitia mwamvuli wa ZURA.
Rais Dk. Shein alisisitiza
kuwa kamwe neema ya MwenyeziMungu hazibezwi, hazizarauliwi na badala yake zinatunzwa
na ujenzi wa jengo hilo ni neema za Mapinduzi hivyo, lazima litunzwe.
Aidha, Dk. Shein
aliitaka Wizara ya Ardi, Nyumba, Maji na
Nishati kupitia ZURA kulikarabati jengo lake Wizara linalotumika hivi sasa mara
baada ya kuhama ili liweze kupendeza na kusaidia kwa mambo mengine.
Aliiambia Bodi ya
ZURA kufanya kazi ya kuwafundisha wafanyakazi wenye uwezo kwa kuwapatia mafunzo
ili wabobee kwenye taaluma kwani Serikali inahitaji wataalamu ambao watatoka
miongoni mwao wa fani zote ambao ZURA itawahitajia.
Aidha, Rais Dk.
Shein alieleza kuwa mara baada ya
kukamilika kwa jengo hilo ambalo tayari ofisi hiyo mara baada ya kukamilika ni
vyema wafanyakazi wa ZURA wakafanya kazi za
nje kwani ujenzi huo utatekeleza haja na hoja ya wafanyakazi kufanya
kazi zao vyema.
Rais Dk. Shein aliitaka
Bodi ya ZURA kutojisahau na kuitaka
kufuata Sheria ya ZURA na utumishi wa Umma ya Namba mbili ya mwaka 2011 kwani ndio nyenzo muhimu ya
kuongoza ZURA na wasiende nje zaidi ya hapo.
Alisema kuwa yeye
hana tatizo na Bodi iwapo itatoa tunza fulani kwa wafanyakazi wa taasisi hiyo
wanapofanya vizuri, ila jambo la muhimu
ni kufuata Sheria na Utaratibu ikiwa ni pamoja na kumshirikisha Waziri husika
wa Wizara hiyo.
Rais Dk. Shein
alisisitiza kuwa Bodi inapotaka
kupandidha mishahara ni vyema iseme na imueleze Waziri na sivyo kama
ilivyofanywa na baadhi ya Bodi ambazo zimechukua madaraka yasio yao na kufanya
makosa makubwa.
Alisema kuwa Bodi
zinafanya kazi kupitia kwa Waziri, na Sheria hizo zipo lakini walikuwa
hawashauriani na ndio maana marekebisho
yanataka kufanya lakini kunakuwa na changamoto kutokana na hali.
Pamoja na hayo,
Rais Dk. Shein alisema kuwa sheria zipo kanuni zipo na kusisitiza kuwepo haja
ya kuwajibika na kuitumia fursa hiyo kukumbusha kuwa kazi iliyopo ni moja
ambayo ni kuwatumikia wananchi wote bila ya ubaguzi wa aina yoyote.
Alisema kuwa yeye
pamoja na viongozi wengine waliochanguliwa
na wananchi ni vyema wakawatumikia wananchi na kufanya kazi kwa pamoja kwani Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar mambo yake mazuri licha ya kuwepo wachache wanaoikejeli.
Alisisitiza kuwa
katika nchi za Afrika Mashariki Zanzibar pekee ndiyo uchumi wake umeweza
kuimarika na kukua kwa asilimia 7.7 mnamo mwaka 2018.
Alieleza
kushwangazwa kwake na wale waliosema
kuwa uchumi wa Zanzibar unaanguka na uko chini lakini hakuwajibu na kama
ilivyo kawaida yake yeye hujibu kwa vitendo.
Aliongeza kuwa
licha ya uchumi mdogo wa Zanzibar lakini bado Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
inaendesha elimu na afya bure.
Alieleza kuwa
jengo hilo linajengwa kwa fedha za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zipatazo
Bilioni 20 ambazo zinatokana na uchumi wa Zanzibar pamoja na miradi mengine
kadhaa inayoendelea kutekelezwa kutokana na uchumi huo huo wa Zanzibar.
Alieleza kuwa
kutokana na mafanikio mbali mbali yaliopatikana Zanzibar pia, kuna nchi
zinakuja kujifunza Zanzibar na kutoa mfano wa Pencheni jamii kwa wazee na
kueleza kuwa katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati ni nchi mbili tu ambazo
zinatekeleza Pencheni hiyo na ipo moja ambayo inajikongoja.
Sambamba na hayo,
Rais Dk. Shein alitoa pongezi kwa Wizara pamoja na ZURA kwa jambo hilo la
ujenzi wa jengo hilo na kuwasisiatiza kuendelea kufanya kazi kwa mashirikiano
hatua ambayo itaimarisha na kuleta manufaa zaidi na mafanikio kwa jumla.
Nae
Waziri wa Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati Salama Aboud Talib alieleza kuwa
juhudi kubwa busara na hekima alizozichukua Rais Dk. Shein ndizo zilizochangia
kuimarika kwa ujenzia wa jingo hilo na kumpongeza kwa miongozo aliyoitoa katika
kuhakikisha jengo hilo linajengwa tena kwa kiwango cha hali ya juu.
Waziri
Salama alitumia fursa hiyo kutoa pongezi zake kwa wafanyakazi wa Wizara yake
kwa kushirikiana pamoja katika
kuhakikisha wanaitekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM.
Alisema
kuwa wafanyakazi wa Wizara yake wamekuwa wakifanya kazi kwa mashirikiano
makubwa miongoni mwao kati yao Wizara,
Bodi pamoja na Idara zake zote na kueleza kuwa anaamini kuwa iwapo malighafi
zote zinazohitajika zitapatikana basi kabla ya kumaliza muda wake Rais Dk.
Shein atalizindua jingo hilo.
Mapema
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba,
Maji na Nishati Alhalil Mirza alieleza kuwa ujenzi wa jengo hilo ni utekeleza Malengo
ya Dira ya Maendeleo ya mwaka 2020 pamoja na kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya
CCM ya mwaka 2015-2020.
Aidha,
alisema kukamilika kwa aujenzi huo kutaondosha changamoto ya eneo la kufanyia
kazi kwa taasisi hiyo ya ZURA.
Alieleza
kuwa Kampuni ya HAINAN International ya China ilikidhi vigezo vilivyotakiwa na
kukubali kuanza kazi za ujenzi ambapo gharama zote za ujenzi huo zinagharamiwa
na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na hadi kumalizika kwake jumla ya TSh
Bilioni 20.2 zinatarajiwa kutumika.
Alisema
kuwa muda wa ujenzi kwa mujibu wa mkataba ni miaka miwili kuanzia Februari 2,
2018 hadi Februari 2020 kwa kufanikisha mambo yote ya msingi ikiwemo kujenga
majengo mawili ya ghorofa ambayo yatakuwa na sehemu ya chini ya ardhi kwa ajili
ya kuegesha magari 50.
Sehemu
nyengine ni ghorofa moja ya chini, ghorofa saba za kwenda juu, lifti mbili,
ujenzi ambao utakuwa kwa zege kwa ghorofa zote pamoja na kuwekwa vifaa vya
usalama, vifaa vya umeme na maji, kupaka rangi na kutengeneza mandhari ya nje
pamoja na bustani kwa mujibu wa mchoro.
Viongozi mbali mbali walihudhuria katika hafla
hiyo akiwemo makamo wa Piliwa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd, ambapo
kabla ya kuweka jiwe hilo la msingi alitembelea ujenzi huo na kupata maelezo
kutoka kwa viongozi wa Wizara pamoja na viongozi wa Kampuni ya HAINAN International
ya China.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024
2231822
E-mail:
rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment