WAZIRI wa Afya,Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoani Tanga Ummy Mwalimu kushoto
akimkabidhi mabati 100 Diwani wa Kata ya Kirare Jijini Tanga Mwagilo
ambazo zitatumika kwa ajili ya ujenzi wa zahanati za Mapojoni na
Ujenzi wa Bweni la Wasichana Shule ya Sekondari Kirare wanaoshuhudia
katikati ni Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudu Mayeji kushoto ni Mkuu
wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa
WAZIRI wa Afya,Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoani Tanga Ummy Mwalimu akiteta jambo
na Mganga wa Mfawidhi wa Zahanati ya Mapojoni mara baada ya kukabidhi
mabati hayo wa pili kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi
Mayeji
WAZIRI wa Afya,Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoani Tanga Ummy Mwalimu akizungumza
mara baada ya kukabidhi mabati hayo kushoto ni Mkurugenzi wa
Jiji la Tanga Daudi Mayeji
WAZIRI wa Afya,Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoani Tanga Ummy Mwalimu kulia
akimsikilkiza kwa umakini Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Mapojoni
wakati alipokwenda kukabidhi mabati 100
WAZIRI wa Afya,Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoani Tanga Ummy Mwalimu kushoto
akikagua dawa kwenye zanhanati ya Mapojoni wakati alipokwenda
kuwakabidhi mabati 100 kwa ajili ya
MBUNGE wa Viti Maalumu mkoani Tanga (CCM) na
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu
leo amekabidhi mabati 100 katika Kata ya Kirare Jijini Tanga kwa ajili
ya zahanati za Mapojoni na Ujenzi wa Bweni la Wasichana Shule ya
Sekondari Kirare
Ujenzi huo wa Bweni la Wasichana kwenye
shule hiyo litasaidia kuondosha changamoto ya watoto kutembea umbali
mrefu kufuata huduma ya elimu umbali wa kilomita 15 jambo ambalo
linaweza kupelekea kukumbana na vishawishi ambavyo vinaweza kukwamisha
ndoto zao.
Halfa ya makabidhiano hayo yamefanyika leo
kwenye Kata hiyo ikiwa ni juhudi kubwa zinazoonyeshwa na Mbunge huyo
kwa ajili ya kuhakikisha changamoto mbalimbali zinazowakabili
wananachi anashirikiana nao kuweza kuzipatia ufumbuzi.
Akizungumza mara baada ya kukabidhi mabati hayo Waziri Ummy alisema
serikali ya awamu ya tano itaendelea kuchapa kazi kwa ufanisi mkubwa
ili kuweza kutatua changamoto wa wananchi ili ziwez kupata ufumbuzi .
Sambamba na Waziri huyo kuchangia mabati hayo wakati huo
huo Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto imeguswa
na changamoto hiyo na kuchangia mabati 50 na saruji 70 katika ujenzi
wa bweni la wasichana la shule ya Sekondari Kirare na kushiriki kwenye
shughuli za ujenzi.
Alisema kwani wao watahakikisha
wanashirikiana na wananchi kwenye maeneo mbalimbali kuona namna ya
kuzipatia ufumbuzi changamoto za Afya ambazo zinaweza kuwa kikwazo
kwenye kujiletea maendeleo.
“Labda niwaambie tu kwamba
Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais wetu Dkt John Magufuli imekuwa
mstari wa mbele kuhakikisha changamoto mbalimbali zinbapatiwa ufumbuzi
hivyo endeleeni kushirikiana nayo kuweza kupata mafanikio “Alisema
Waziri Ummy.
Aidha pia Waziri huyo alisisitiza umuhimu wa
wananchi kuhakikisha wanakata bima za Afya ili ziweze kuwasaidia
kunufaika na huduma za matibabu wanapokuwa wakiugua.
“Niwasisitize kwamba kateni bima ya Afya mkiumwa muweza kupata
huduma za matibabu kwani wengine fedha zenu ni za msimu hivyo mkiwa na
bima mnaweza kupata matibabu bure”Alisema
Waziri huyo
alisema kwani gharama za matibabu zimekuwa kubwa hivyo iwapo
wakijiunga na bima hususani iliyoboreshwa ukitoa elfu thelathini kwa
kaya ya watu sita unaweza kupata huduma za matibabu kwenye maeneo
mbalimbali.
“Bima kubwa ya kitaifa ya NHIF wanabima ya
mtoto wameona badala ya kusema mtoto aishie elfu thelathini tu kwa
hiyo ukimliptia mtoto 50400 atapata huduma mzuri”Alisema
Alisema sababu ya kusaidia juhudi hizo za wananchi ni kutokana na
kuguswa namna walivyojitahidi kuhakikisha wanajenga jengo hilo
mkishirikiana na viongozi wenu namna nikaona bora niwaunge mkono.
Aidha alisema anaamini mabati hayo yatakuwa chachu katika
kutatua changamoto iliyopo kwenye jengo hilo ili kuweza kuzimaliza na
kutoa fursa kwa wananchi kuweza kupata huduma bila kuwepo vikwazo.
“Lakini hapa nimeambiwa mnachangamoto ya vifaa hivyo
nitashirikiana nanyi kuweza kuzipatia ufumbuzi vifaa vyote
vinavyoihitaji kwenye zanahati hii”Alisema
Awali akiz
Mganga Mkuu wa Jiji la Tanga (CMO) Isango Isubiri alisema wanamshukuru
Rais John Magufuli kwa kutoa fedha za ukarabati za vituo vya afya
kwenye Jiji ambavyo ni Makorora,Ngamiani,Mikanjuni na Duga ambao kwa
sasa unaendelea.
Alisema kwenye zahanati ya Mapojoni
Jijini Tanga kulikuwa na uhaba wa chumba cha maabara na daktari hivyo
kilichofanywa na Waziri huyo ni kutambua umuhimu kuunga mkono nguvu
za wananchi katika ujenzi wa jengo hilo lenye uhitaji mkubwa ambalo
baada ya kulijenga walikosa mabato na saruji ili kuweza kulikamilisha.
Mganga huyo wa Jiji alisema ujenzi wa Jengo hilo ulianza
mwaka 2016 ambapo litakapokamilika litakuwa msaada mkubwa kwa wananchi
ambao wanakwenda kupata huduma za matibabu kwenye zahanati hiyo.
Aidha alisema pia suala lingine ni ujenzi wa hospitali ya
wilaya ya Tanga ambapo zilitolewa Bilioni 3.6 katika kipindi cha mwaka
2018 jambo ambalo limesaidia kuweza kuondosha changamoto ya afya.
No comments:
Post a Comment