Habari za Punde

Tanga Uwasa Yakabidhiwa Vifaa Vya Ujenzi Vyenye Thamini ya Shilingi Milioni 10 Kwa Shule ya Sekondari ya Mkwakwani


MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa  katikati akipokea vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya sh.milioni 10 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa kwenye shule ya Sekondari Mikanjuni kutoka kwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Rahma Msofe kulia jana ambao walikabidhi vifaa hivyo  ili viweze kutumika kwenye ujenzi huo ili kupunguza uhaba wa vyumba vya madarasa shuleni hapo wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly wa pili kutoka kulia ni Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha Salim



MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa  katikati akipokea vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya sh.milioni 10 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa kwenye shule ya Sekondari Mikanjuni kutoka kwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Rahma Msofe kulia jana ambao walikabidhi vifaa hivyo  ili viweze kutumika kwenye ujenzi huo ili kupunguza uhaba wa vyumba vya madarasa shuleni hapo wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly wa pili kutoka kulia ni Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha Salim
MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akizungumza katika hafla hiyo ya makabidhiano
Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka hiyo Rahma Msofe akizungumza kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini  Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly akizungumza katika halfa hiyo
Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga (DAS) Faidha Salimu akizungumza katika halfa hiyo
 Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Dorrah Killo akizungumza katika halfa hiyo
Afisa Elimu Taaluma Jiji la Tanga akizungumza katima hafla hiyo
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Mikanjuni  Kaana Erasto akitoa taarifa ya shule hiyo
 Sehemu ya wanafunzi wa shule hiyo
 Sehemu ya walimu wa shule hiyo wakifuatilia halfa hiyo ya makabidhiano
 Sehemu ya walimu wa shule hiyo wakifuatilia halfa hiyo ya makabidhiano
 Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Dorrah Killo kulia akiamkaribisha Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa mara baada ya kuwasili kwenye viwanja vya shule ya Sekondari Mikanjuni
 MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa kiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kamabidhiano hayo
 Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini  Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly akiwaongoza viongozi mbalimbali wakati walipotembelea ujenzi wa vyumba vya madarasa kwenye shule ya Sekondari Mikanjuni
 Sehemu ya watumishi wa Tanga Uwasa wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Tanga
 MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akiagana na watumishi wa mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) mara baada ya kumalizika kwa halfa hiyo kulia ni Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha Salim

 Sehemu ya Kokoto zilizokabidhiwa
MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa kushoto akitokea nondo 60 kwa ajili ya ujenzi kutoka kwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Rahma Msofe kulia ni  Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini  Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly

MAMLAKA ya Maji Safi na Usafiri wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) imekabidhiwa vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya milioni 10 kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa madarasa kwenye shule ya sekondari Mikanjuni ikiwa ni mkakati wa kuunga mkono juhudi za Serikali kuondosha changamoto zinazoikabili sekta hiyo.

Halfa ya makabidhiano hayo ilifanyika kwenye shule hapa baina ya Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka hiyo Rahma Msofe na Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa wakiwemo Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo Mhandisi Geofrey Hilly na Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha Salim.

Vifaa vilivyokabidhiwa shuleni hapo kwa ajili ya kumalizia madarasa matatu ni pamoja na saruji mifuko 100, nondo 60, shehena za kokoto, mchanga, mbao, waya na vifaa vingine vyot ambavyo vitasaidia ujenzi huo ili kutoa fursa wanafunzi kupata fursa ya kusoma bila kuwepo kwa vikwazo vyovyote.

Akizungumza mara baada ya kutokea msaada huo wa vifaa hivyo vya ujenzi Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa alipongeza juhudi ambazo zimefanywa na mamlaka hiyo kwa kusaidia kuondosha changamoto za elimu kwenye shule hiyo.

Mwilapwa alisema juhudi ambazo zimefanywa na mamlaka hiyo zinapaswa kuungwa mkono na mashirika ya Umma na makampuni binafsi kuhakikisha yanachangia masuala ya elimu ili kuunga mkono juhudi za serikali katika kukabiliana na uhaba wa madarasa.

Mkuu huyo wa wilaya alisema serikali inakabiliwa na changamoto kubwa hasa katika sera yake ya elimu bure kutokana na idadi ya wanafunzi wanaofaulu toka darasa la saba kwenda kidato cha kwanza kuongezeka siku hadi siku na kupelekea uhaba wa vyumba vya madarasa.

Alisema mamlaka hiyo mbali na jitihada za kuimarisha huduma ya maji nam usafi wa mazingira Jijini Tanga pia imechukua dhamana ya kuimarisha miundombinu ya shule hiyo ambayo inauhitaji wa madarasa kutokana na ongezeko la wananfunzi.

Awali akizungumza katika halfa hiyo ya makabidhiano Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka hiyo Rahma Msofe alisema kilichofanywa na Mamlaka hiyo ni sehemu ya kuchangiaji wa huduma za kijamii ili kumuunga mkono Rais Magufuli katika harakati zake za kuiboresha elimu.

Msofe alisema vifaa vilivyotolewa shuleni hapo kwa ajili ya kumaliziamadarasa matatu ni pamoja na saruji mifuko 100, nondo 60, shehena za kokoto, mchanga, mbao,waya na vifaa vingine vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 10.

“Malengo yetu si kuhudumia sekta ya maji tu bali tutaendelea kujikita katika kusaidia huduma za kijamii pale tutakapoona upo ulazima wa kufanya hivyo bila ya kuathiri utendaji wa kazi zetu”Alisema Msofe.

Awali akisoma taariafa fupi mbele ya mgeni rasmi Mkuu wa Shule hiyo Kaana Erasto alisema shule hiyo iliyo na wanafunzi 1319 inauhitaji wa madarasa 33 huku yaliyopo 24 ambapo kunaupungufu wa vyumba 9 ili kutoa fursa kwa wananfunzi kupata sehemu ya kujisomea.

Alisema jitihada za wadau zimeanza na tayari ujenzi wa vyumba vitatu kati ya tisa umekwisha anza na majengo yapo katika hatua za mwisho ili kuweza kukabiliana na uhaba huo na kutoa fursa kwa wanafunzi ambao wamekosa mahala pa kujisomea.

Erasto alisema wanafunzi waliopata nafasi ya kujiunga na shule hiyo kidato cha kwanza mwaka 2019 ni 405 huku 150 ndio waliopo madarasani ambapo wanafunzi 255 wakikosa mahala ma kujisomea na kupelekea wahisani kujitolea katika ujenzi wa madarasa.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.