Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino Bw.
Athmani Masasi akisisitiza umuhimu wa
wananchi wa Wilaya ya Chamwino hasa Vijiji vilivyopatiwa mafunzo ya kuwajengea
uwezo baada ya kurasimisha mashamba yao na
kupatiwa hati za haki miliki za kimila za kumiliki ardhi ikiwa ni sehemu
ya jitihada za Serikali kuwakwamua wakulima ili waweze kuzalisha kwa tija.
Mafunzo hayo yameratibiwa na Ofisi ya Rais, Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na
Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA).
Meneja
Urasimishaji Ardhi Vijijini kutoka Ofisi ya Rais, Mpango wa
Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) Bw. Anthony
Temu akiwaasa wananchi wa Wilaya ya Chamwino kutumia fursa zinazojitokeza baada
ya kurasimisha mashamba yao ili kuongeza tija, Mafunzo hayo yakuwaongezea ujuzi ni moja ya mkakati wa Serikali kuwakwamua
wakulima baada ya kurasimisha mashamba yao.
Sehemu
ya wakulima wa Kijiji cha Mahama
Wilayani Chamwino wakifuatilia mafunzo
ya kuwajengea uwezo ili waweze kuongeza tija katika uzalishaji baada ya mafunzo
yaliyoendeshwa na Ofisi ya Rais, Mpango
wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) kwa
kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino.
Kikundi
cha ngoma kikionesha umahiri wake wakati wa hafla ya kufunga mafunzo kwa
wakulima zaidi ya 100 wa kijiji cha Mahama Wilayani Chamwino. Mafunzo yaliyoendeshwa na Ofisi ya Rais, Mpango wa Kurasimisha
Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) kwa kushirikiana na
Halmashauri ya Wilaya hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji
wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino Bw. Athmani Masasi akiwa kwenye picha
ya pamoja na sehemu ya wakulima walioshiriki
katika mafunzo yakuwajengea uwezo ili waweze kuzalisha kwa tija.
(Picha
zote na Frank Mvungi- Dodoma)
Na;
Frank Mvungi- MAELEZO, Dodoma
Wananchi Wilayani Chamwino Wameaswa Kufanya Kazi kwa
Bidii ili kuendana na azma ya Serikali ya Awamu ya Tano kuwaletea wananchi
maendeleo kwa kutumia rasilimali zilizopo katika maeneo yaoikiwemo Ardhi.
Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo kwa wakulima zaidi
ya mia moja wa kijiji cha Mahama Wilayani humo, Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashauri ya Wilaya hiyo Bw. Athmani Masasi amesema kuwa wananchi wote
wanapaswa kuunga mkono juhudi za Serikali
kwa kufanya kazi kwa kufuata mfano wa Mhe. Rais, Dkt. John Pombe
Magufuli ili ili kufikia maendeleo endelevu.
"
Hati za haki milki ya kimila
zimepunguzwa bei kutoka elfu ishirini
hadi elfu mbili mia saba tu ili kila mwananchi wa Wilaya ya Chamwino aweze
kuunga mkono juhudi za Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuwaletea wanyonge
maendeleo na kuwakwamua kiuchumi" Alisisitiza Masasi
Akifafanua
amesema kuwa Halmashauri hiyo itaendelea kuweka mikakati yakuwezesha wananchi
wote wanamiliki maeneo yaliyopimwa na kuwa rasmi kwa ajili ya shughuli za
kiuchumi hali itakayosaidia kuongeza kasi ya maendeleo.
Pia
alipongeza Ofisi ya Rais, Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za
Wanyonge Tanzania (MKURABITA) kwa hatua inazochukua katika kuwajengea uwezo
wananchi ili waweze kuwa na uzalishaji wenye tija hasa kupitia urasimishaji wa
mashamba yao.
Kwa upande wake Meneja Urasimishaji Ardhi
Vijijini kutoka MKURABITA Bw. Antony
Temu amesema kuwa wakulima wa kijiji cha Mahama wamewezeshwa kutekeleza dhana
ya kilimo chenye tija, ufugaji wa
kisasa, utunzaji wa kumbukumbu, utafutaji wa fursa na kuzitumia, utunzaji
kumbukumbu, namna ya kukuza mitaji, ushirika na utunzaji wa mazingira.
Aliongeza
kuwa Dhamira ya MKURABITA ni kuona wananchi wanakuwa na ustawi unaotokana na
rasilimali zilizopo katika maeneo yao ikiwemo ardhi.
Aidha,
alimshukuru Mhe. Rais, Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuendelea kuwezesha mpango huo kutekeleza
jukumu la kuwawezesha wananchi kiuchumi ili wachangie katika kujenga uchumi wa
viwanda kwa kuzalisha malighafi zenye ubora kupitia sekta ya kilimo.
MKURABITA imewajengea uwezo wakulima zaidi ya mia mbili
katika Vijiji vya Mahama na Membe ambapo kila kijiji kilifanikiwa kutoa
wakulima mia moja kushiriki katika mafunzo hayo yaliyolenga kuwapa ujuzi wa
kuongeza tija katika sekta ya kilimo.
No comments:
Post a Comment