Waziri wa Mambo
ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Paramagamba Kabudi akihutubia katika siku ya kumbukumbu ya Mashujaa waliojenga reli ya
TAZARA, wakati wa zoezi la kuweka mashada ya maua iliyofanyika leo (Ijumaa April 5,
2019), katika makuburi ya mashujaa hao yaliyoko Gongo la Mboto Jijini Dar es Salaam,
waliosimama kulia ni Balozi wa China Nchini Tanzania, Wang Ke akiwa pamoja na viongozi kutoka Serikali ya Jamhuri ya Watu wa
China na Tanzania.
Waziri wa Mambo
ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Paramagamba Kabudi (kulia), akipata maelezo kuhusu Mashujaa waliojenga reli ya TAZARA,
katika maadhimisho ya kumbukumbu ya mashujaa hao yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam leo
(Ijumaa April 5, 2019), kushoto ni Balozi wa China Nchini Tanzania, Wang Ke akiwa pamoja na viongozi wengine wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa
China na Tanzania.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Paramagamba Kabudi (kulia), akipata maelezo kuhusu Mashujaa waliojenga reli ya TAZARA, katika maadhimisho ya kumbukumbu ya mashujaa hao yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam leo (Ijumaa April 5, 2019), kushoto ni Balozi wa China Nchini Tanzania, Wang Ke akiwa pamoja na viongozi wengine wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China na Tanzania.Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Paramagamba Kabudi (kulia), akipata maelezo kuhusu Mashujaa waliojenga reli ya TAZARA, katika maadhimisho ya kumbukumbu ya mashujaa hao yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam leo (Ijumaa April 5, 2019), kushoto ni Balozi wa China Nchini Tanzania, Wang Ke akiwa pamoja na viongozi wengine wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China na Tanzania.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Paramagamba Kabudi (kulia), akipata maelezo kuhusu Mashujaa waliojenga reli ya TAZARA, katika maadhimisho ya kumbukumbu ya mashujaa hao yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam leo (Ijumaa April 5, 2019), kushoto ni Balozi wa China Nchini Tanzania, Wang Ke akiwa pamoja na viongozi wengine wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China na Tanzania.
Waziri wa Mambo
ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Paramagamba Kabudi (kulia) na Balozi wa
China Nchini Tanzania, Wang Ke (kushoto) wakiweka mashada ya maua katika moja ya makaburi ya Mashujaa waliojenga reli ya TAZARA katika maadhimisho ya siku ya mashujaa hao iliyofanyika leo
(Ijumaa April 5, 2019) Jijini Dar es Salaam.
Na Paschal
Dotto-MAELEZO
Ushirikiano wa
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Zambia na Jamhuri ya Watu wa China, Wazadi kuimarika kutokana na uwepo
wa miundombinu ya ushafirishaji kupitia Tanzania Zambia Railway TAZARA, iliyojengwa
kwa ushirikiano wa Tanzania, Zambia na China mwaka 1975.na Wasisi wa mataifa hayo ni Mwalimu Julius Nyerere (Tanzania), Dkt. Kenneth Kaunda (Zambia) na Mao ze Dong Rais wa Jamhuri ya Watu wa
China.
Waziri wa Mambo ya
Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Paramagamba kabudi,leo ameongoza
maadhimisho ya kumbukizi ya Mashujaa waliojenga reli ya TAZARA, ambapo yamefanyika katika makaburi ya mashujaa hao yaliyoko
Gongo la Mboto, Jijini Dar es Salaam.
Akielezea historia ya
reli hiyo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof.
Paramagamba Kabudi alisema Ujenzi wa reli hiyo ni muhimu kwa sababu, Benki ya
Dunia wakati huo walikataa kujenga wakisema haukuwa na faida, kadhalika nchi za Ulaya zilikataa zikidai
ujenzi huo haikuwa na faida, Lakini taifa
la wakina likawa tayari kujenga.
“Mwalimu Julius Nyerere, Dkt. Kenneth Kaunda Rais wa Zambia
pamoja na Mao ze Dong Rais wa Jamhuri ya Watu wa China waliamua kujenga reli
hii, siyo kwamba China walikuwa tajiri sana kama walivyo sasa, hapana walifunga
mkanda, kwa hiyo siku ya leo ni muhimu sana kiuchumi, kiutamaduni na
kijamii”, Prof. Paramagamba kabudi ,
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amekumbushia Prof. Kabudi alisema
kuwa katika maadhimisho ya mwaka huu, ni
muhimu kwa Tanzania, kwani kwa sasa China ina mpango wa kutekeleza mradi mkubwa
uitwao Sea Belt and Road Initiatives
unaolenga ujenzi wa miundombinu kuunganisha Afrika, Asia, Ulaya kwa
kutumia miundombinu ya barabara, ndege pamoja na reli ambapo Tanzania itapata
ushirikiano mzuri katika masuala ya usafiri wa anga.
Aidha Prof. Kabudi
alisema kuwa katika maadhimisho ya mwaka marejeo yataweza kuimarisha
ushirikiano na kuwa ni msingi bora wa kuanzisha mahusiano mapya, hususani
katika usafiri wa anga na akaongeza kuwa mwaka huu Shirika la ndege la Tanzania
litaanza safari zake toka Dar es Salaam mpaka Wanzhu Nchini China.
“kwa sisi mwaka huu
sherehe hii ni muhimu sana, kwani tunatarajia kuanza safari za ndege yetu Air
Tanzania kuruka moja kwa moja kutoka Dar es Salaam mpaka Wanzhu nchini China,
hivi karibuni yaweza kuwa mwaka huu (utekelezaji) katika taratibu zote
zitakamilika na safari zitaanza rasmi.”, Prof. Paramagamba WaziriKabudi
aliongeza kuwa safari hiyo ya ndege ya Air Tanzania itaongeza idadi ya watalii kuwa
wengi kuja Tanzania kutoka China, wafanyabiashara kutoka ndani na nje na kuweza
kwenda moja kwa moja Wanzhu, akasema pia wawekezaji kutoka China watawezesha
Serikali kupata mapato mengi.
Kwa upande wake
Balozi wa China nchini Tanzania, Wang Ke alisema kuwa siku ya kumbukizi kwa
mashujaa wa ujenzi wa reli ya TAZARA ni siku muhimu na kwamba inaleta kumbukumbu ya uhusiano kati ya nchi
hizo tatu.
“hii ni siku maalumu
kwa sababu ni siku ya kuadhimisha kumbukizi ya kufa kwa mashujaa wetu hawa,
Mainjinia pamoja na wataalamu mbalimbali walioshiriki katika ujenzi huu, na kufariki,
na hili adhimisho limefanyika hapa Tanzania kwa sababu tunaushirikiano wa muda
mrefu tangu ujenzi wa reli mwaka 1975”, Balozi wa China, Wang Ke alisema.
Wang Ke alisema kuwa maadhimisho
hiyo ni msingi mzuri wa kujenga uhusiano na ushirikiano kati ya Tanzania,
Zambia na China kwani maadhimisho hayo yanatukumbusha matumizi ya reli ya TAZARA
katika ukombozi wa nchi za Kusini mwa Afrika, ikiwemo Zambia.
No comments:
Post a Comment