Habari za Punde

WAZIRI HAROUN ATOA TUZO KWA WAANDISHI WA HABARI WALIOSHINDA UANDISHI WA HABARI ZA RUSHWA ZANZIBAR

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora Haroun Ali Suleiman(wapili kulia) akimkabidhi Tuzo ya Cheti na Laptop Mshindi wa Kwanza wa Uwandishi wa Makala ya Rushwa katika magaazeti Salum Vuai wa Habari Maelezo Zanzibar katika hafla ya Utoaji wa Tuzo ya Waandishi wa Habari kuhusiana na Rushwa na Uhujumu Uchumi ambayo imeandaliwa na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar(ZAECA)iliofanyika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mazizini mjini Unguja.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora Haroun Ali Suleiman(wapili kulia) akimkabidhi Tuzo ya Cheti na Laptop Mshindi wa Kwanza wa Uwandishi wa Makala ya Rushwa katika Vipindi vya Redio Asha Hamad Saleh wa Chuchu FM katika hafla ya Utoaji wa Tuzo ya Waandishi wa Habari kuhusiana na Rushwa na Uhujumu Uchumi ambayo imeandaliwa na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar(ZAECA)iliofanyika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mazizini mjini Unguja.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora Haroun Ali Suleiman(wapili kulia) akimkabidhi Tuzo ya Cheti na Laptop Mshindi wa Kwanza wa Uwandishi wa Makala ya Rushwa katika Vipindi vya TV Online Ameir Khalid katika hafla ya Utoaji wa Tuzo ya Waandishi wa Habari kuhusiana na Rushwa na Uhujumu Uchumi ambayo imeandaliwa na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar(ZAECA)iliofanyika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mazizini mjini Unguja.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora Haroun Ali Suleiman akitoa hotuba katika hafla ya Utoaji wa Tuzo ya Waandishi wa Habari kuhusiana na Rushwa na Uhujumu Uchumi ambayo imeandaliwa na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar(ZAECA)iliofanyika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mazizini mjini Unguja.
Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi(ZAECA)Mussa Haji Ali akizungumza katika hafla ya Utoaji wa Tuzo ya Waandishi wa Habari kuhusiana na Rushwa na Uhujumu Uchumi ambayo imeandaliwa na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar(ZAECA)iliofanyika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mazizini mjini Unguja.
Muakilishi kutoka UNODC Mohamrd Jaafar kutoka Kenya akizungumza machache katika hafla ya Utoaji wa Tuzo ya Waandishi wa Habari kuhusiana na Rushwa na Uhujumu Uchumi ambayo imeandaliwa na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar(ZAECA)iliofanyika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mazizini mjini Unguja.
Baadhi ya Waandishi wa Habari waliohudhuria katika hafla ya Utoaji wa Tuzo ya Waandishi wa Habari kuhusiana na Rushwa na Uhujumu Uchumi ambayo imeandaliwa na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar(ZAECA) iliofanyika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mazizini mjini Unguja.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora Haroun Ali Suleiman ameitaka Mamlaka ya kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar (ZAECA) kuwakamata na kuwafikisha katika vyombo vya sheria wale wote watakaojihusisha na Rushwa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi.
Amesema imezoeleka kuelekea katika kipindi cha Uchaguzi watu wengi hujihusisha na Rushwa hivyo ni jukumu la ZAECA kuwafikisha katika vyombo hivyo ili sheria ichukuwe mkondo wake.
Waziri Haroun ameyasema hayo alipokuwa akikabidhi Tunzo za washindi wa habari za Rushwa katika hafla iliyofanyika Hotel ya Zanzibar Beach mjini Zanzibar.
Amesema ni wakati sasa Zanzibar kuiga mfano wa nchi ya China ambako nchi hiyo haina uvumilivu kwa watu wanaojihusisha na Rushwa.
“Wenzetu China wana zero tolerance kwa watu wanaojihusisha na Rushwa, na hayo ndio mambo ya kuiga” alisema Waziri Haroun.
Aidha amewataka Waandishi wa habari kuandika habari zitakazofichua vitendo vya rushwa vinavyoisumbua jamii.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Yakuti Hassan Yakuti amefahimisha kuwa kwa sasa taarifa za Rushwa zinapewa umuhimu katika vyombo vya habari hivyo ni vyema waandishi wakaendeleza kuzianidika kwa kina zaidi.
Awali akitoa taarifa kuhusiana na Tunzo hiyo Mkurugenzi wa ZAECA Mussa Haji amefahamisha kuwa Ofisi yake huzipa umuhimu wa kipekee na kuzifanyia kazi taarifa za Rushwa zinazotoka katika vyombo vya habari.
Kwa upande wake Mwakilishi Muhammed Jafar  kutoka Taasisi ya UNODC kutoka Kenya  amewataka Waandishi wa habari kuandika habari ambazo zinazogusa maisha ya Wananchi wa kawaida.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.