Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Mhe, Vuai Mwinyi akizunguma na kutoa shukrani kwa Wananchi wa Mkoa huo, wakati wa Hafla ya futari ilioandaliwac na Rais wa Zanzibar kwa Wananchi wa Nkoa wa Kaskazini katika Ukumbi wa Chuo Cha Amali Mkokotoni Unguja.
WANANCHI wa Mkoa wa Kaskazini Unguja waeleza kuridhishwa
na juhudi za Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali
Mohamed Shein katika kuwapelekea maendeleo endelevu ikiwemo miundombinu ya
barabara.
Ameendelea kuwasisitiza wafanyabiashara kutowauzia
wananchi bidhaa kwa bei ya juu katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani na miezi
ijayo.
Akitoa neno la
shukurani kwa niaba ya Rais Dk. Shein, Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Vuai
Mwinyi, aliyasema hayo katika futari maalum iliyoandaliwa na Rais Dk. Shein kwa
ajili ya wananchi wa Mkoa huo, futari iliyofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Amali
Mkokotoni Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Katika maelezo yake
Mkuu huyo wa Mkoa alieleza kuwa wananchi wa Mkoa huo wamekuwa wakishuhudia
maendeleo makuwa yanayopelekwa na
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya uongozi wa Rais Dk. Shein.
Mkuu huyowa Mkoa alielezaku
wa miongoni mwa wananchi ambao
hawatamsahau Rais Dk. Shein katika maisha yaokutokana na kuviimarishavijiji
vyao kwa kuvipelekea huduma za maendeleo zikiwemo maji, umeme, skuli, barabara
na vituo vya afya.
Akivitaja vijiji hivyo
kikiwemo kijiji cha Mlilile, Mgonjoni, Mbuyumaji na vyenginevyo Mkuu huyo wa
Mkoa alieleza kuwa wananchi wa vijiji hivyo wamefarajika kwa kupata huduma hizo
muhimu za maendeleo ambazo walizikosa kwa muda mrefu.
Aidha, Mkuu huyo wa
Mkoa aliendelea kutoa shukurani hizo kwa huku akieleza jinsiwananchi wa Mkoa
huo walivyo na matarajio makubwa ya kukua kwa uchumi wao kutokana na ujenzi wa
barabara ya Bubu hadi Mkokotoni ambayo inaendelea na ujenzi.
Alisema kuwa
kukamilika kwa barabara hiyo kutawasaidia kwa kiasi kikubwa wananchi wa Mkoa
huo katika kukuza uchumi wao sambamba na kukuza uchumi wa Taifa.
Sambamba na hayo, Mkuu
huo wa Mkoa huo alitoa ongezi kwa Rais Dk. Shein kwa kuendeleza utamaduni wake
wa kuwafutarisha wananchi jambo ambalo alisema lina baraka na rehema kubwa mbele
ya Mwenyezi Mungu.
Pamoja na hayo, Mkuu
wa Mkoa huo wa Kaskazini Unguja aliwasisitiza wananchi wa Mkoa huo kuendeleza
umoja na mshikamano wao ili maendeleo zaidi yazidi kupatikana.
Pia, alitumia fursa hiyo kutoa shukurani kwa
niaba ya Rais Dk. Shein kwa wananchi wote waliohudhuria katika futari hiyo
aliyowaandalia na kupongeza jinsi walivyoonesha upendo mkubwa kwake wa kukubali
muwaliko wake huo.
Wakati huohuo, nae Mama Mwanamwema
Shein kwa upande wake aliungana na akina mama wa Mkoa huo pamoja na viongozi
wanawake wa kitaifa katika futari hiyo maalum aliyoianda Rais Dk. Shein huko
katika ukumbi wa Chuo hicho cha Amali Mkokotoni.
Katika hafla hiyo ya
futari viongozi mbali mbali walihudhuria akiwemo Makamo wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Balozi Seif Ali Idd na viongozi wengine wa dini na Serikali pamoja na
wananchi mbali mbali wa Mkoa huo.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment