Habari za Punde

Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar Afanya Ziara Kisiwani Pemba Kutembelea Miradi ya ZUSP.

MKURUGENZI wa Baraza la Mji Wete Hamad Mbwana Shehe, akitoa maelezo ya baraza lake kwa Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar Balozi Moahemd Ramia Abduwawa, wakati alipotembelea miradi ya ZUSP Pemba, ikiwemo ujenzi wa ofisi ya baraza la mjini Wete, Standi ya magari na soko la Wete
WAZIRI wa Fedha na Mipango Zanzibar Balozi Mohamed Ramia Abduwawa, akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika baraza la Maji Wete, wakati wa ziara yake ya siku mbili Kisiwani Pemba kuangalia utekelezaji wa miradi ya ZUSP, aliyesimama ni mkurugenzi wa baraza hilo Hamad Mbwana Shehe

WAZIRI wa Fedha na Mipango Zanzibar Balozi Mohamed Ramia Abduwawa, akimsikiliza kwa makini Afisa Mdhamini Wizara hiyo Ibrahim Saleh Juma (kulia) akitoa maelezo juu ya soko la wate, wakati balozi Ramia alipotembelea ikiwa ni miongoni mwa miradi mikubwa ya ZUSP
WAZIRI wa Fedha na Mipango Zanzibar Balozi Mohamed Ramia Abduwawa katika, akimsisitiza jambo Mkurugenzi wa baraza la Mji Wete Hamad Mbana Shehe , wakati alipofanya ziara ya kutembelea mradi ya ZUSP ikiwemo soko la wete, maduka ya wafanya biashara na stendi ya magari
MUONEKANO wa Ofisi ya Baraza la Mji Wete ambayo imejengo kupitia mradi wa ZUSP, kama inavyoonekana ikiwa inapendeza.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.