Waziri wa Viwanda na Biashara,
Innocent Bashungwa akizungumza wakati wa hafla ya kufunga Manoesho ya 43 ya
Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) yanayoendelea katika Viwanja vya
Mwalimu Julius Nyerere leo Alhamisi (Julai 11, 2019).
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akizungumza wakati akiyafunga Maonyesho ya 43 ya Biashara ya Dar es salaam Tanzania yanayofanyika katika Ukumbi wa Rashid Mfaume Kawawa ndani ya Uwanja wa Mwalimu Julius K. Nyerere.
01. Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya
Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd akimkabidhi cheti cha ushindi mmoja wa
washiriki wa makampuni kutoka nchini Rwanda, wakati wa hafla kufunga Manoesho ya 43 ya Biashara ya
Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) leo Alhamisi (Julai 11, 2019)yanayoendelea
katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere.
01. Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya
Mapinduzi, Balozi Seif Alli Idd akimkabidhi cheti cha ushindi mmoja wa
washiriki wa makampuni yaliyoshiriki katika Maonesho ya 43 ya Biashara ya
Kimataifa Dar es Salaam wakati hafla
kufunga maonesho hay oleo Alhamisi (Julai 11, 2019) yanayoendelea katika
Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere.
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya
Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Alli Idd akimkabidhi cheti cha ushindi Afisa
Habari Mwandamizi wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Bi Dorina Kaaya wakati
wakati wa hafla kufunga Manoesho ya 43
ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) leo Alhamisi (Julai 11,
2019)yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere.
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya
Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Alli Idd akimkabidhi cheti cha ushindi mmoja wa
washiriki kutoka Kampuni ya uzalishaji maziwa ya Asasi Diaries wakati wakati wa
hafla kufunga Manoesho ya 43 ya Biashara
ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) leo Alhamisi (Julai 11, 2019)yanayoendelea
katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere.
(PICHA NA PASCHAL DOTTO-MAELEZO)
Na
Mwandishi Wetu
MAELEZO
MAKAMU wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi
Zanzibar, Balozi Seif Iddi ameitaka Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania
(TANTRADE) kuendelea kuimaisha mitandao na mifumo ya biashara nchini ili kuwawezesha
wafanyabiashara wa Tanzania kuweza kuwa na uhakika wa masoko bora ya bidhaa za ndani
na nje ya nchi.
Akifunga
Maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) leo Alhamisi
(Julai 11, 2019) Balozi Idd alisema Maonesho hayo ya mwaka huu yameonesha
dhamira na mwelekeo wa Serikali katika kutumia fursa biashara na viwanda katika
kujenga uchumi imara pamoja na kutengeneza ajira kwa wananchi.
Balozi
Idd alisema ni wajibu wa TANTRADE kutumia fursa za uwepo wa makampuni ya
wazalishaji, wauzaji na wafanyabiashara kutoka nje wanaoshiriki katika maonesho
hayo kuweza kujenga mitandao imara ya mahusiano na ushirikiano kwa wafanyabiashara
wa ndani ili kuweza kuwatafutia masoko ya bidhaa zao ambazo kwa sasa zimeanza
kuzalishwa katika viwango bora nchini.
“Nawapongeza
TANTRADE kwa juhudi zenu za kuanzia klinilki za biashara, na hili limewezesha
wafanyabiashara wetu kuweza kukutana na wanunuzi mbalimbali ambao huweza kuwapa
uzoefu wa namna bora zaidi ya kuzalisha bidhaa zenye kukithi viwango na ubora
unaotakiwa” alisema Balozi Idd.
Aidha
Balozi Idd alisema Serikali kwa sasa inatekeleza Mpango Kazi wa Kuboresha Mfumo
Udhibiti wa Biashara Nchini (Blue Print), ambao umekusudia kuondoa changamoto
mbalimbali za wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi, hivyo aliitaka TANTRADE
kushirikiana na wadau na wazalishaji wa sekta binafsi ili kuiwezesha sekta ya
biashara kuvutia wawekezaji wengi zaidi.
Kwa
mujibu wa Balozi Iddi pia aliitaka TANTRADE kuweka utaratibu wa kufuatilia oda
za maombi mbalimbali zinazotolewa na wafanyabiashara kutoka nje ya nchi ili
kuendelea kupanua wigo wa soko la bidhaa za Tanzania nje ya nchi ambalo kwa
sasa limeendelea kupanuka kutokana na juhudi mbalimbali zinazofanywa na
Serikali.
Balozi
alisema ni wajibu wa Watanzania kujenga utamaduni wa kuthamini bidhaa za ndani
ili kuziwesha kupata masoko ya uhakika kwa kuwa kwa kufanya hivyo kutatoa fursa
ya kuweza kutambulika kwa haraka pamoja na kumudu changamoto ya ushindani wa
masoko ya bidhaa zinazozalishwa nje ya nchi.
Alisema
kuwa maonesho hayo ya 43 yamethibitisha uwezo wa wafanyabiashara wa Tanzania
katika kutengeneza na kuzalisha bidhaa
mbalimbali kwani idadi ya washirki wa maonesho kutoka nje ya nchi imeweza kuongezeka
kutoka makampuni kutoka nje 2956 mwaka 2018 hadi kufikia 3250 mwaka 2019, hivyo
kudhibitisha uwezo wa serikali katika kusimamia sekta ya biashara nchini.
Balozi
Idd anasema kuwa Makampuni ya wafanyabiashara ya Tanzania yaliyoshiriki
maonesho hayo yanapaswa kupata uzoefu na uelewa mkubwa katika namna bora zaidi
ya kusimamia na kuratibu sekta ya biashara nchini katika viwango bora ili
kuweza kutengeneza masoko ya uhakika katika nchi za nje.
Kwa
upande wake Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa alisema Serikali
imeendelea kuboresha mazingira ya biashara nchini ikiwemo kuanza kufanya
mapitio ya sera na sheria mbalimbali ambazo awali zilikuwa zikileta changamoto
mbalimbali kwa wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi.
Aliongeza
kuwa katika kuhakikisha kuwa sekta ya viwanda na biashara inaleta tija katika
ukuaji uchumi nchini, Serikali imekusudia kuweka msisitizo katika kujenga
uchumi jumuishi kwa kuziweka sekta ya uvuvi, kilimo na mifugo kuwa kipaumbele
muhimu katika kuzitumia rasilimali mbalimbali zilizopo katika sekta hizo katika
kutengeneza ajira kwa wananchi walio wengi.
No comments:
Post a Comment