Habari za Punde

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Balozi Seif Ali Iddi Aongoza Dua na Hitma ya Marehemu Dr. Badria Masjid Mushawar Muembeshauri Zanzibar.ONGOZA DUA YA HITMA YA DK.BADRIYA

 MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd,akiongoza Kisomo cha Hitma ya Marehemu Dk.Badriya Abubakar Gurnah aliyekuwa Mke wa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi, kilichofanyika katika Msikiti wa Mwushawal Mwembe Shauri Unguja.
 WAUMINI mbali mbali wa Dini ya Kiislamu wakishiriki Kisomo cha Hitma ya Marehemu Dk.Badriya Abubakar Gurnah, kilichofanyika katika Msikiti wa Mwushawal Mwembe Shauri Unguja.
NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi, akiwashukru Waumini wa Dini ya Kiislamu wakiwemo Viongozi wa Dini,Serikali,Chama Cha Mapinduzi na Wananchi wote walioshiriki Kisomo cha Hitma ya Mkewe Marehemu Dk.Badriya Abubakar kilichofanyika Msikiti wa Mwushawal Mwembe Shauri Unguja.




NA IS-HAKA OMAR,ZANZIBAR.
MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd, ameongoza Kisomo cha Hitma ya Mke wa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi Marehemu Dk.Badriya Abubakar Gurnah kilichofanyika katika Msikiti wa Mwushawal uliopo Mwembe Shauri Unguja.
Kisomo hicho kimeudhuriwa na Waumini wa Dini ya Kiislamu,Viongozi wa Dini,Kiserikali na Chama Cha Mapinduzi pamoja na Wananchi kwa ujumla.
Akitoa Mawaidha Sheikh Norman Jongo, amewasihi Waumini hao kuendelea kumuombea dua mara kwa mara Marehemu Dk.Badriya ili awe miongoni mwa Waja Wema katika Pepo ya Mwenyezi Mungu.
Akitoa shukrani Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Mabodi, amewashukru Wananchi walioshiriki katika kisomo hicho na harakati zingine za kumsaidia Dk.Badriya Enzi za Uhai wake.
Sambamba na hayo pia amewashukuru Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Joseph Magufuli kwa mchango walioutoa kabla na baada ya Kifo cha Dk.Badriya.
Wakati huo huo Wananchi,Viongozi wa Dini ya kiislamu, Kiserikali na Chama cha Mapinduzi kwa upande wa Wanawake nao wameshiriki kisomo hicho cha Hitma ya Dk.Badriya Abubakar hapo Nyumbani kwa Dk.Mabodi  Mtaa wa Raha leo Unguja.
Mwenyezi Mungu amlaze mahala Pema Peponi Amin.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.