Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein akiwa Ofisini kwake Ikulu Zanzibar akiangalia Meli Mpya ya Mafuta ya MT.Ukombozi II ikiwasili Zanzibar ikitokea Nchini Shanghai China ilikoundwa na Kampuni ya Damen Shipyard ya Uholanzi.
HATIMAE ahadi ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza
la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein aliyowaahidi wananachi wa Zanzibar kuwa
Serikali anayoiongoza itanunua meli mpya ya mafuta MT. UKOMBOZI II leo imetimia
baada ya meli hiyo kuwasili katika Bandari ya Zanzibar ikitokea Shanghai nchini
China.
Rais Dk. Shein akiwa
Ofisini kwake Ikulu mjini Zanzibar alipata fursa ya kuiona meli ya MT UKOMBOZI
II ikiwasili kutoka ukingoni mwa pwani ya Zanzibar ikitokea usawa wa kisiwa cha
Chumbe na kuelekea katika Bandari ya Malindi Mjini Unguja ilipokwenda kutia
nanga.
Akiwa katika varanda ya jengo la Ikulu mjini Zanzibar Rais Dk.
Shein alionekana akiwa na furaha kubwa wakati akiiangalia meli hiyo ikiwasili
ikiwa ni kutokana na ahadi aliyoitoa na azma yake juu ya ujio wa meli hiyo mpya
ya mafuta.
Meli hiyo
iliyotengenezwa na Kampuni ya Damen Shipyardya nchini Uholanzi iliwasilirasmi katika
Bandari ya Malindi Zanzibar majira ya saa saa tano za asubuhi na kupata
mapokezi ya aina yake.
Wafanyakazi wa Wizara
hiyona viongozi wao pamoja na wafanyakazi wa taasisi nyengine za Serikalina
sekta binafsi waliungana pamoja na baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria
katika eneo la Bandari ya Malindi mjini Zanzibar kwa ajili ya mapokezi ya meli
yao hiyo.
Mapema hapo jana Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi,
mawasiliano na Usafirishaji Ndg.Mustafa Aboud Jumbe akitoa taarifa kwa wananchi huko ofisi kwake Kisauni,
alithibitisha ujio wa meli hiyo na kueleza jinsi hatua mbali mbali zilizochukuliwa katika mchakato wa kununuliwa meli hiyo na Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar hadi kuwasili kwake hapa nchini hii leo.
Kwa maelezo ya Katibu Mkuu huyo meli mpya MT UKOMBOZI II,
ni meli mpya ambapo majadiliano juu ya ujenzi wa meli hiyo yalianza mwaka 2017 na mkukuku wake
uliwekwa rasmini mwezi Julai mwaka 2018 na hatimae meli hiyo ujenzi wake ulimalizika mwezi
April mwaka huu.2019.
Katibu Jumbe katika taarifa yake alisema kwamba hivi karibuni ujumbe kutoka Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar ulikwenda kuishuhudia meli hiyo mnamo Julai 8, 2019 ikiwa tayari imeshakamilika na ndipo wakafanya makubaliano na watengenezaji wa meli hiyo ya Kampuni ya
DAMEN TANKER SHIP ya Uholanzi iliyoitengeneza meli hiyo.
Ndg.Jumbe alieleza kuwa baada ya makubaliano hayo Meli hiyo iliaza
safari ya kusafiri kutoka bandari ya Shanghai nchini China kwa muda wa siku 28 na kuwasili hapo jana katika maji ya pwani ya Zanzibar
na leo iliwasili kwa makabidhiano rasmina Serikali na baada ya hapo itazinduliwa kwa ajili ya kuanza shughuli iliyokusudiwa.
Alieleza kuwa meli hiyo ni meli ya mafuta yenye urefu wa mita 86.2
na yenye uwezo wa kupakia tani 3,500 za mafuta kwenye visima 4 vilivyomo katika meli hiyo.
Aidha thamani iliyotumika kuitengeneza meli hiyo ni URO
Milioni 14.3 sawa na wastani wa Bilioni 36 za Kitanzania ambapo meli hiyo itaungana na meli ya MT
UKOMBOZI I ambayo ipo hapa nchini na yenye uwezo wa kupakia tani 2,400.
Katibu Mkuu huyo alieleza kuwa madhumuni ya taarifa hiyo aliyoitoa hapo jana jioni ni kuwaarifu wananchi kuwa meli hiyo imeshawasili
Zanzibar na maandalizi yanafanywa ili izinduliwe rasmini tayari ameshaombwa Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa meli hiyo katika siku itakayopangwa.
Aliwashukuru wananchi wa Zanzibar
kwa kufuatilia kwa makini juu ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015-2020
kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kama ilivyo elezwa kwenye ukurasa wa 152 kifungu
cha 90 katika kifungu kidogo cha 4
ambacho kimeagiza kwamba Serikali itanunua meli mpya ya mafuta kwa ajili ya matumizi ya
Zanzibar.
“Naomba sana kumshukuru Mhe.Rais kwa kutuamini kuisimamia kazi hiyo na hivi sasa tuko ukiongoni katika kuikabidhi meli hiyo”,alisema Ndg.Mustafa Jumbe.
Hizo ni juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
chini ya uongozi wa Rais Dk. Shein katika kuhakikisha sekta ya usafiri na usafirishaji inaimarika kwa kiasi kikubwa ambapo mnamo mwezi Disemba mwaka
2015 meli mpya ya MV MAPINDUZI IIiliwasili Zanzibar ikitokea nchini Korea
Kusini ilikotengenezwa ikiwani agizo la Rais Dk. Shein la kununuliwa meli hiyo.
MV MAPINDUZI II ambayo ilitengenezwa na Kampuni ya
Daewoo International ya nchini Korea Kusini ilianza kutengenezwa Julai mwaka 2013
na hadi Disemba 2015 iliwasili Zanzibar ikiwa tayari kuanza kutumika.
Jumla ya Dola za Marekani 30.4
zilitumika kutengenezea meli hiyo ambapo ujenzi wake hadi kukamilika ulichukua miezi 18 ambapo meli hiyo ya
MV MAPINDUZI II inauwezo wa kuchukua abiria 1200 pamoja na tani 200 z amizigo.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
No comments:
Post a Comment