Na.Paschal
Dotto-MAELEZO 21-08-2019
Mkurugenzi Mkuu wa
Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt.Hassan Abbasi ametoa
mafunzo kwa watumishi wa Shirika la Reli Tanzania TRC kuhusu umuhimu wa
mawasiliano kimkakati katika miradi mikubwa inayotekelezwa na Serikali.
Katika mafunzo hayo,
Dkt.Abbasi amesema kuwa ili miradi mikubwa iweze kujulikana kwa wananchi,
Taasisi husika zinapaswa kuzingatia misingi mikubwa minne katika kuandaa habari
ili kuwahabarisha wananchi kuhusu miradi hiyo, akakumbusha;
Katika kutekeleza
ahadi zake kwa wananchi, Serikali ilitoa Fedha za utekelezaji wa ujenzi wa Reli
ya kisasa (SGR) ambapo TRC inapaswa kutangaza mradi kwa wananchi, akasema,
“kuna
misingi minne ambayo inapaswa kutekelezwa ili kuwezesha mawasiliano ya
kimkakati katika mradi huo ambao wananchi wanapaswa waujue”, Dkt.Abbasi.
Msemaji Mkuu huyo wa
Serikali aliitaja misingi hiyo kuwa ni Maono katika kuwahabarisha wananchi (Pro-Active),
akaeleza kuwa ili wananchi waweze kujua kinachoendelea katika mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa (SGR), TRC ambayo inakabidhiwa fedha nyingi za
walipa kodi,haina budi kuonesha zinavyotumika.
Msingi mwingine Dk.
Abbasi ametaja kuwa ni Ujumbe unaotolewa
(Messaging)
katika kutekeleza kufikisha ujumbe kwa wananchi, akasema, TRC inapaswa kuwaeleza wananchi kwa mahususi kuhusu mradi huo kuwa
utakuwa na manufaa na faida gani kwa fedha zao.
Akaongeza kuwa katika
kuutangaza maradi huo, TRC wanapswa kuwa na mawasiliano baina ya wao na taasisi
au wadau wao (Collaborations) ili hatimaye kubainisha kwa wananchi
wayasemayo ili kuwezesha upatikanaji wa habari sahihi, hapa alisema wataalum
katika kada mbalimbali kwenye Taasisi wanapaswa kushiriki kimkakati kutoa takwimu
za kitaalamu kwa Afisa Habari ili aweze kuzinyambua kabla ya kuzipeleka kwa wananchi au walengwa.
Alitaja msingi
mwingine ni kuweza kutanua wigo kwa kutumia Vyombo mbalimbali Kuhabarisha (Multi-Media) hii ni dhana ya kutumia njia nyingi za habari, kuhabarisha wananchi hasa mitandao ya kijamii,magazeti, radi na
runinga, na kuwatumia wataalum wa kada ya Habari kwa kuandaa picha, Video na Graphics, kuandika habari na makala ili kurahisisha mtazamaji au msomaji kuelewa
haraka kwa njia hizo na hivyo kuuelewa mradi wa SRG.
“Taasisi za Serikali
mnapaswa kuwekeza zaidi kwenye kitengo cha habari, ikiwemo kuwa na wataalamu
mbalimbali katika kada hii, lakini mnatakiwa muwe hasa kwenye mitandao ya
kijamii”
Akaeleza kuwa nusu ya
watu duniani wako kwenye mitandao ya kijamii kwa sasa, na kwamba jitihada
zinaendelea za kubadilisha Taasisi mbalimbali kutoka kutegemea gazeti la kesho
badala ya pia kutumia mitandao ya kijamii ambako taarifa zinafika kwa haraka na
kwa uhakika zaidi kwa watu wengi.
Aidha, Dkt. Abbasi
alitembelea ujenzi wa Stesheni mpya ya reli ya kisasa SGR ambapo alielezwa
ujenzi wa reli unaendelea vizuri, na akawataka watanzania kuiunga mkono
Serikali ili kutekeleza kwa pamoja ujenzi wa Reli hiyo na akasema,”reli hii itakuwa
na manufaa kwa vizazi vya leo, kesho na vijavyo”.
Kwa upande wake
Mkurugenzi Mkuu waTRC, Masanja Kadogosa alisema kuwa katika kutekeleza masuala
ya kuwajuza wananchi kuhusu mradi huo, Idara ya Habari ni muhimu na amemshukuru
Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO kuwatembelea na kuwapa darasa katika
masuala ya mawasiliano kimkakati kwenye mradi wa SGR.
“Siku zote tunasema
huu ni mradi mkubwa sana ambao Serikali inautekeleza ndani ya nchi yetu, na
wananchi hawa wakati wote wanahitaji kuhabarishwa manufaa ya mradi huu, kwa
hiyo ujio wa Msemaji Mkuu wa Serikali kwetu sisi ni faraja ya kupata uzoefu
mkubwa kwenye masuala ya Habari”, alisema Kadogosa.
Mkurugenzi Mkuu wa
Shirika la Reli Tanzania (TRC) Masanja Kadogosa akifafanua hatua za ujenzi wa
Stesheni mpya ya reli ya kisasa(SRG) kwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO
na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt.Hassan Abbassi, alipotembelea Ofisini hapo leo
Agosti 21, 2019, kutoa mafunzo ya
umuhimu wa sekta ya mawasiliano katika kutangaza miradi ya Serikali.
Mkurugenzi wa Idara
ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt.Hassan Abbassi, akieleza
jambo kwa Waandishi wa Habari (hawapo pichani), kuhusu utekelezaji wa ujenzi wa
Stesheni mya ya reli ya kisasa(SRG), alipotembelea Ofisini hapo.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania
(TRC) Masanja Kadogosa akifafanua jambo kwa Waandishi wa Habari (Hawapo
Pichani) kuhusu kuhusu utekelezaji wa ujenzi wa Stesheni mya ya reli ya
kisasa(SRG), alipotembelewa na Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji
Mkuu wa Serikali, Dkt.Hassan Abbassi Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Idara
ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt.Hassan Abbassi, katika picha
ya pamoja na Manajimenti ya wafanyakazi wa Shirika la Reli Tanznaia ( TRC)
alipofika Ofisini hapo leo Agosti 21, 2019,
kutoa mafunzo ya umuhimu wa Sekta ya Mawasiliano katika kutangaza miradi
ya Serikali.
No comments:
Post a Comment