RAIS wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk.
Ali Mohamed Shein ameitaka jamii kuzingatia umuhimu wa kuwaheshuimu na
kuwatendea wema wazee, kwa kutambuwa kuwa ni misingi muhimu ya silka, malezi na
utamaduni wa Wazanzibari.
Dk. Shein amesema hayo leo
katika ufunguzi wa mkutano mkuu wa Jumuiya ya Wazee na Wastaafu Zanzibar
(JUWAZA), uliofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idris Abdul wakil, Kikwajuni
mjini hapa.
Amesema jamii imekumbwa
na vitendo vya udhalilishaji na
unyanyapaa dhidi ya wazee, huku kukiwa na watu ndani ya familia
wanaowadharau wazee wao kwa kuwatukana pamoja na kuwahusisha na imani za kuwashirikina na dhana za kuhusika na vitendo viovu, ikiwemo
uchawi na wanga.
Alisema kuna baadhi ha
vijana mbali na kusomeshwa vyema na wazee wao, wamekuwa wakiwadharau wazee kwa
kigezo kuwa hawaendani na hadhi walizonazo, mambo yanayochangia na kuwafanya
wazee kukosa amani, matunzo, misaada na haki wanazostahiki.
“Haki ya kuheshimiwa na
kutunzwa ni ya msingi kwa kila mzee, vijana wana wajibu wa kuwapa wazee wao
haki zao kwani huo ni wajibu wao”, alisema.
Aliitaka jamii kuendelea
kuwaheshimu wazee kutokana na mambo mbali mbali makubwa waliyolifanyia Taifa na
kusisistiza haja ya kuendelea kuwatunza
an kuwaenzi ili kupata fursa ya kuchota hekima na busara kutoka kwao.
Alisema nchi zote zinazoendelea
zimekuwa na utamaduni wa kuwaenzi na kuwathamni wazee na wastaafu na kuwatumia
ipasavyo, hususan pale kunapohitajika ushauri wa mambo mbali mbali, kutokana
ana maarifa, hekima na uzoefu wao katika masuala ya kimaisha.
Aidha, alisema ni muhimu
kuzingatia suala la kuwatunza wazee kuwa limetiliwa mkazo katika mafunzo ya
Dini zote, ikiwa ni hatua maalum katika kuwatendea wema.
Dk. Shein alisema katika
kudhihirisha dhamira njema ya Serikali katika kuyashughulikia masuala ya wazee,
mara baada ya Mapinduzi matukufu ya 1964, Rais wa kwanza wa Zanzibar, hayati
Abeid Amani Karume alianzisha ujenzi wa nyumba za wazee kwa lengo la
kuwahifadhi, hususan wale waliokosa uwezo na watu wa kuwahudumia.
Alisema Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar imekuwa ikiendeleza utaratibu wa kuwapa hifadhi na
kushughulikia changamoto mbali mbali zinazowakabili wazee, kwa kutambuwa kuwa
huo ni wajibu wake wa msingi.
“Lazima tuwathamini wazee
wetu, tuwaheshimu na tuwahifadhi kwa kusikiliza shida zao na kuzitafutia
ufumbuzi kwa kadri ya uwezo wetu”, alisema Dk Shein.
Aidha, alibainisha kuwa
wajibu wa kuyashughulikia masuala yanayowahusu waze ni hatua ya utekelezaji wa
Ilani ya CCM ya uchaguzi mkuu wa 2015 – 2020, kama ilivyoainishwa katika Ibara
ya 135,
Dk. Shein alieleza taarifa
ya Idadi ya watu na iliofanyiika mwaka
2012 imebainishwa kuwepo zaidi ya wazee 53, 311 wenye umri wa kuanziza miaka
60, hatua iliyoifanya Serikali kuanzisha Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, wazee,
wanawake na watoto baada ya kutambua thamani yao..
Aidha, alisema Serikali
ilianzisha Sera ya Hifadhi ya Jamii mnamo mwaka 2014, kwa lengo la kusimamaia
wazee wote nchini, ikiwemo wenye umri wa kuanzia miaka 70 na kuendelea na
kuwapatia posho la shilingi 20,000 kila mwezi.
“Serikali itaendelea
kuyaimarisha makaazi yao na kuhakikisha kuwa wazee hao wanapewa huduma zote
muhimu wanazostahili, zikiwemo za chakula, matibabu, maji safi na salama pamoja
na ulinzi wa maisha yao”, alisema.
Dk. Shein aliweka wazi
malengo ya serikali ya kuwapatia wazee hao mazingira bora zaidi ya kuishi ikiwa
pamoja an kuwaandalia ziara za kuzitemebelea sehemu mbali mbali za kihistoria
na za maendeleo.
Alisema amefurahishwa
sana mafanikio makubwa yaliopatikana kupitia JUWAZA kutokana na kazi kubwa ya
kuwaunganissha wazee kwa lengo la kuimarisha hali zao kiafya, kiuchumi na
ustawi bora wa maisha yao.
Akigusia maomba mbali
mbali yaliowasilishwa kwake, Dk. Shein alisema Serikali inalifanyia kazi ombi
la kuongeza kiwango cha posho ya Pensheni
jamii na kuahidi kulitolea uamuzi kutegemea na wakati husika.
Sambamba na hilo, Dk.
Shein alisema ni jambo zuri kuwepo kwa sheria, itakayozingatia mambo mbali
mbali ya wazee, huku akionyesha imani kubwa aliyonayo ya Rais ajaye kuendelea
na ataratibu wa utoaji wa Pensheni jamii kwa kuzingatia kuwa atakuwa na uelewa
mpana wa Ilani ya CCM.
Aidha, Dk. Shein
alikubali kuwa mlezi wa Jumuiya ya Wazee na Wastaafu (JUWAZA) pamoja na kuunga
mkono rai ya uanzishaji wa mfuko maaalum, ili kusaidia shughuli mbali mbali za
kuendeleza Jumuiya hiyo.
Katika hatau nyengine,
Dk. Shein alipokea Cheti cha Uongozi bora kutoka JUWAZA pamoja kupokea Kadi ya
Uanachama wa Jumuiya hiyo.
Nae, Waziri wa Wizara ya
Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na watoto Modline Castico, alisema kuwepo kwa
mswada wa sheria kuhusiana na utoaji wa Pensheni jamii, umewafanya wazee
kufurahia jambo hilo, kwa kuzingatia kuwa utawahakikishia ulinzi wa haki zao,
sambamba na kuondokana na vitendo vya udhalilishaji.
Alisema Wizara hiyo
itaendelea na juhudi zake za kupigania
na kuimarisha haki na ustawi bora wa maisha ya wazee nchini.
Mapema, akisoma Risala ya
Jumuiya hiyo, Amour Haji Nassor aliiomba Serikali kuangalia uwezekano wa kuongeza
kiwango cha Posho la Pensheni jamii kwa
wastani wa asilimia hamsini ya kima cha chini cha mshahara, kabla ya kumaliza
kwa awamu ya saba ya Uongozi.
Aidha, alipongeza juhudi
kubwa zinazochukuliwa na Serikali katika kuwapatia wazee huduma mbali mbali za
kijamii, ikiwemo suala la afya bora , akibainisha juhudi hizo zimefanikiwa
kuimarisha hali zao.
Abdi Shamna, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422
Tel.:0777476982. Fax: 024 2231822
E-mail: abdya062@gmail.com
No comments:
Post a Comment