Makamanda walioguswa na mabadiliko hayo
ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Zimamoto (SACF) Hamis Telemkeni, aliyekuwa Mkuu
wa Kitengo cha Monitoring and Evaluation Makao Makuu Dodoma, anakwenda kuwa
Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji (RFO) Mkoa wa Tanga.
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Zimamoto
(SACF) Goodluck Urio, aliyekuwa Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (RFO)
Mkoa wa Tanga, anakwenda kuwa Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Morogoro.
Aliyekuwa Kamanda wa Jeshi la Zimamoto
na Uokoaji (RFO) Mkoa wa Iringa, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Zimamoto (SACF)
Ambwene Mwakibete, anakwenda kuwa Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa
Mwanza, nafasi yake inachukuliwa na Mrakibu Msaidizi wa Zimamoto (ASF) Isabela
Mbwago.
Vilevile Mrakibu Msaidizi wa Zimamoto
(ASF) Jumbe Kondo, anakwenda kuwa Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji (RFO) Mkoa wa
Njombe.
Pia aliyekuwa Kamanda wa Jeshi la Zimamoto
na Uokoaji Mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi wa Zimamoto (ACF) Gilbert Mvungi,
amehamishiwa Makao Makuu ya Zimamoto na Uokoaji Dodoma.
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linaendelea
kutoa wito kwa Wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Makamanda wa Zimamoto
na Uokoaji Mikoa na Wilaya katika suala la Kinga na Tahadhari Dhidi ya majanga
na maokozi.
Imetolewa
na;
Joseph
Mwasabeja – (INSP)
Msemaji wa Jeshi
la Zimamoto na Uokoaji
Makao Makuu
3 Septemba, 2019
www.frf.go.tz www.twitter.com/tanzimamoto www.instagram.com/zimamoto_uokoaji www.facebook.com/frf.tz
No comments:
Post a Comment